TFF kufungua mashtaka dhidi ya mitandao ya kijamii...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limemwagiza mwanasheria wake kufungua mashtaka kwa wale waliosambaza taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuichafua taasisi hiyo. Matukio360 haimo katika sakata hilo.
Katikati ni Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo inakuja baada ya jana kusambaa  taarifa za kuwatuhumu viongozi wa TFF kuongeza posho kwa wajumbe wa kamati ya utendaji pamoja na kuanzisha malipo ya mishahara kwa rais na makamu wake.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa TFF Wilfred Kidao alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

“Ninamwagiza mwanasheria wetu kufungua mashtaka kwa wale waliosambaza ujumbe kwenye mitandao ya kijamii wenye lengo la kuichafua taasisi,” amesema Kidao.

Aidha amekanusha taaarifa hizo kwa kusema kuwa viwango vya posho za vikao vya Kamati ya Utendaji havijawahi kujadiliwa wala kubadilishwa.

Ameongeza kwamba wajumbe wa kamati ya utendaji wanawezeshwa sh.milioni 1.5 kwa miezi mitatu ili kuwasaidia katika kutgrkrleza majukumu yao.

Akitolea ufafanuzi kuhusu malipo ya Rais na Makamu wake, amesema suala hilo halikufikiwa mwafaka na kamati ya utendaji hivyo walishauri rais ahudumiwe na TFF kama ilivyo kwa marais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CUF).

Pia Kidao amebainisha kuwa Rais wa TFF Wallace Karia alikataa kwa kusema, anaamini sio wakati mwafaka wa yeye kuchukua posho hadi taasisi itakapokaa vizuri na taratibu zote kufuatwa
    .


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search