Nusu wanafunzi elimu ya juu wakosa mikopo…Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Salha Mohamed
MTANDAO wa Wanafunzi Tanzania(TSNP) umesema nusu ya wanafunzi wenye sifa na waliodahiliwa  na vyuo vya elimu ya juu nchini wamekosa mikopo na kurudi nyumbani.


Mkurugenzi wa Idara ya haki mtandao wa wanafunzi Abdul Nondo(katikati) akitoa msimamo wa taasisi hiyo katika suala la utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu leo jijini Dar es Salaam. 

Pia umetoa siku tano kwa Serikali kuhakikisha wanatoa tamko na azimio walioamua juu ya wanafunzi  wenye sifa, waliokosa mikopo  ili waweze kudahiliwa na kuanza masomo.

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo na Mkurugenzi wa Idara ya Haki TSNP, Abdul Nondo wakati akizungumza na waandishi wa habari na kutoa msimamo wa mtandao huo katika suala la utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Amesema serikali ilipanga kutoa sh bilioni 427 kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kwa wanafunzi wote nchini ambapo kwa mwaka wa kwanza ilipanga kutoa sh bilioni 108.8 kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza sawa na wanafunzi 30,000.

“Wanafunzi waliodahiliwa mwaka huu ni elfu 61, hii inamaanaisha kwa vyovyte vile wanafunzi elfu 31 kati ya elf 61 walioomba mkoo walipaswa kukosa mkpo, tunashangazwa na Bodi ya mikopo kupitia mkurugenzi wake kuwa walichambua wasiokuwa na sifa lakini wanafunzi hao hawakukosa mkopo kutokana na vigezo bali ni idadi iliyowekwa,”amesema.

Amefafanua kuwa serikali inapaswa kufanya kama ilivyofanya sekondari kwa kulipa ada ya kila mwanafunzi  huku mzazi akigharamia chakula na malazi.

“Hadi jana tumepata taarifa kuna baadhi ya vyuo wanafunzi wanarudi nyumbani kutokana na kukosa ada na hawaruhusiwi kuingia darasani kwani hawajasajiliwa na chuo,”amesema.

Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza mkazi wa mkoani Kilimanjaro, Denis Shirima amesema si kwamba bodi ya mikopo imewanyima mkopo kutokana na kukosa vigezo. 

Amesema ameambatanisha nyaraka zote zinazomthibitishia kuwa yeye ni Yatima na anapaswa kupata mkopo lakini amekosa. 

"Najua wapo wengi kama mimi wamekosea mkopo mkono na hawana ndugu hapa jijini, wengine wmejishikiza tu kwa marafiki zao akitegemea mkopo lakini amefika amekuta hajapata, "amesema. 

Amesema wapo wanafunzi wanaorudi majumbani mwao kutokana a kushindwa kulipa ada jambo linalosababisha kukosa kudahiliwa chuoni n kukosa masomo. 

" Mwanzo tulipofika chuo tulikuwa tunaibia ibia tu kuingia darasani ili tupate mwanga wa kile tulichoomba kusoma lakini sasa hivi haruhusiwi kuingia hadi uwe na kitambulisho na hadi kupewa lazima uwe umelipa ada, "amesema. 
Amesema anatarajia kupata kauli kutoka kwa waziri wa elimu, Profesa Joyce Ndalichako kwani hadi sasa hawana mwelekeo huku masomo yameanza vyuoni.,"amesema.

Naye mwanafunzi wa Maka wa pili katika chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Aziza Rashidi amesema mwaka wa kwanza aliomba mkopo lakini alikosa ambapo alifika bodi ya mikopo ambapo maofisa wa bodi hiyo walishangaa kukosa mkopo kwani alikuwa anavigezo vya kupata. 

"Mwaka wa kwanza nimesoma kwa kuomba na kukupa kwa ndugu ndugu na jana jana na sasa hivi na dawa nikaomba tena mwaka huu sijapata sina wazazi nimeweka dhamana vyeti vyangu ili nipate hela niseme na sijapata mkopo, "amesema. 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

1 comment

  1. TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
    SAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
    NA BINAFSI
    MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
    philipmorganloanservice00@gmail.com

    JAZA NA URUDI

    Jina:
    Kiasi cha Mkopo:
    Muda:
    Jinsia:
    Nchi:
    Lengo:
    Namba ya simu ya mkononi:

    JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA

    ReplyDelete

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search