Vigogo wanne Tanesco wafikishwa mahakamani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki

WAFANYAKAZI wanne wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na wengine wawili leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na Mashtaka 202 ya uhujumu uchumi na kusababisha hasara ya bilioni 2.7.

Wafanyakazi hao wa Tanesco  ni Mhasibu Mwandamizi wa Mapato, Emmilian Mlowe, Assistant office Automation, Shakila Ngella, Meneja Mwandamizi wa Fedha, Mkama Maira na Mhasibu anayeshughulikia madeni, Yaled Jonas.

Wengine wanaokabiliwa na kesi huyo ni  Bashiru Ngella na Barnabas Massaly.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa leo amewasomea washtakiwa hao Mashtaka  kwa kusaidiana na Wakili wa Serikali,Gloria  Mwenda mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Kishenyi amedai kati ya Januari 7, 2014 na Januari 31,2015 Dar es Salaam walikula njama ya kutenda makosa ya wizi.

Amedai  katika kipindi hicho, washtakiwa, Emilian, Shakila, Mkama na Yared wakiwa waajiliwa wa Tanesco Kinondoni wakiwa na uwezo wa kuingia katika mfumo wa kompyuta unaojulikana kama Tansms33 kwa nia ya kulaghai walifanya maingizo ya uongo katika mfumo huo ya kiasi cha  Sh 2,746,485,545.63 wakijaribu kuonyesha zililipwa kwa Tanesco  na mawakala wa tatu kama manunuzi ya umeme wa Luku (unit).

Wakili Kishenyi na Wakili Mwenda waliwasomea washtakiwa hao kwa kupokezana kuanzia  shtaka la 3 hadi la 201 ambayo yote ni ya wizi wa mamilioni ya fedha, fedha ambazo ni Mali ya Tanesco.

Katika shtaka la 202 washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka la kusababisha hasara.

Wanadaiwa kuwa kati ya Julai Mosi ,2014 na Machi 31,2016 washtakiwa hao kwa matendo yao waliisababishia Tanesco kupata hasara ya Sh 2,746,485,545.63.

Baada ya kusomewa Mashtaka hayo washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza hadi Mahakama Kuu.

Upande wa Mashtaka alidai kuwa upelelezi wa kesi huyo bado haujakamilika na wakaomba ipangiwe tarehe ya kutajwa.

Hakimu Nongwa aliwashauri washtakiwa hao kuomba dhamana katika Mahakama Kuu kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi maarufu Mahakama ya Mafisadi.

Washtakiwa wamepelekwa rumande na kesi imeahirishwa hadi Novemba 21,2017. Washtakiwa hao wanawakilishwa na mawakili Ruben Simwanza na Gidion Opanda

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search