Utendaji wa waziri Lukuvi mhh!!!...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na  mwandishi wetu
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi  ameelezea utendaji wake wa miaka miwili tangu ateuliwe nafasi hiyo


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akiongea wakati wa uzindua wa miradi ya upatikanaji wa picha za anga na mfumo unganishi wa menegiment ya taarifa za umma (ILMIS) jijini Dar es Salaam hivi karibuni

Amesema  lengo la Serikali ni kupima kila kipande cha ardhi  nchini na  hati za kimila 46,000 zimetolewa na Serikali

Mapato ya Serikali yameongezeka kutoka milioni 46 hadi bilioni 100 kutokana na mifumo dhabiti ya ukusanyaji Kodi

Migogoro zaidi ya Elfu 30 imetatuliwa kati ya migogoro 62,529 iliyopokelewa Katika Mabaraza ya Ardhi nchini.

Amesema muda wa kupata Hati umepungua kutoka siku 90 hadi 30 tangu maombi kupokelewa

Makazi zaidi ya 20,040 yametambuliwa na kurasimishwa. Serikali inakamilisha sera ya Ardhi iliyozingatia maoni ya wadau

Pia  Serikali imeunda kanda 8 ili kuongeza tija katika kuwahudumia wananchi.Wizara yake imenunua vifaa vipya na vya kisasa vya upimaji ardhi ili kuboresha utendaji katika kanda ilizounda

Mashamba zaidi ya 150 yamefutiwa Hati kwa kuwa hayakuwa yameendelezwa ili yatumike na wananchi

Kampuni 61 zimesajiliwa ili kusaidia upimaji wa ardhi  nchini na kwamba kama umekopa fedha ili kuendeleza shamba lazima utumie kwa kusudi hilo tu na si vinginevyo

Amesema wizara yake sasa imeanza kujenga mifumo ya kielektroniki ili kudhibiti taarifa  za ardhi  na  kuanzia mwakani taarifa za ardhi zitakuwa katika mfumo wa kielektroniki utakaondoa udanganyifu

Kanzi Data ya taarifa za ardhi imeshajengwa  na mfumo wa kielektroniki utaunganishwa na mifumo ya NIDA



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search