StarTimes yaja na 'Mfalme wa Familia'...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Star Media (T) Ltd kupitia chapa yake ya StarTimes katika msimu huu wa Sikukuu imekuja na Ofa ya aina yake ijulikanayo kama ‘Mfalme wa Familia’ kwa ajili ya wateja watakaopenda kujiunga na huduma za kampuni hiyo.
Meneja Uhusiano na Masoko wa kampuni hiyo Juma Suluhu.
Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam na  Meneja Uhusiano na Masoko wa kampuni hiyo Juma Suluhu akizungumza na waandishi wa habari, amesema  StarTimes inatambua umuhimu na uzito wa kipindi hiki cha sikukuu kwa watanzania hivyo wamejipanga vyema kutoa burudani ya kiwango cha hali ya juu.

“Tumewaletea watanzania Ofa tuliyoipatia jina la ‘Mfalme wa Familia’, tumeiita hivyo kwa sababu sisi ni wafalme wa Burudani za Familia, ukianzia filamu, michezo kama mpira wa miguu, kikapu, katuni, Muziki, Ndondi na vingine vingi. Tuna vipindi ambavyo watoa huduma wengi hawana, hivyo ni fursa ya kipekee kwa watanzania kufurahia,” amesema Juma.

Aidha ameongeza kuwa ofa hiyo inaenda sambamba na kushuka bei ya king’amuzi cha Antenna ambacho awali kilikuwa kikiuzwa kwa Tsh 47,000 ambacho kwa wakati hua kitapatikana kwa bei ya punguzo ya sh. 34,000 .

“Ofa yetu ina mambo makubwa matatu, Jambo la kwanza ni hilo punguzo la bei ya king’amuzi cha Antenna, pili ni king’amuzi cha Combo ambacho kinatumia dish na Antenna ambacho awali kilikuwa kikiuzwa kwa Tsh 86,000 sasa kitapatikana kwa Tsh 78,000 huku mteja atakayenunua atapata kifurushi cha Mwezi mzima pamoja na Dish Bure”, amesema Juma.

“Tatu ni luninga zetu za kidigitali, hapa unapata vitu vitatu, cha kwanza luninga zetu zina king’amuzi ndani, cha pili ukinunua luninga yetu unapatiwa dish bure na cha mwisho utaunganishwa kifurushi cha Uhuru kwa mwezi mmoja Bure”, ameongeza.

Licha ya ofa hizo wateja wa StarTimes wataweza kupata Chaneli zote za Kifurushi cha Kili katika kifurushi cha Uhuru kuanzia Disemba 1, 2017 ikiwa ni sehemu ya Promosheni ya Mfalme wa Familia ambayo imeletwa na StarTimes Tanzania.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search