Wanaokufa kwa kisukari waongezeka...soma habari kamili na Matukio360..#share
Salha
Mohamed
IMEELEZWA ifikapo mwaka 2030 ugonjwa wa kisukari nchini unakadiriwa
kusababisha vifo vitokanavyo na magonjwa
yasiyoambukiza kwa asilimia 7.
Waziri, Ummy mwalimu
Makadirio
hayo yametolewa jijini Dar es Salaam mwenyekiti wa muungano
wa vyama vya magonjwa yasiyoambukiza Tanzania(TANCDA), Tatizo Waane na kuwa
kisukari ni ugonjwa unaokuwa kwa kasi duniani.
Pia
amesema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy
Mwalimu anatarajia kuwa mgeni rasmi katika matembezi ya kujenga ufahamu wa
uwepo wa ugonjwa wa kisukari nchini.
Matembezi
hayo yatafanyika Novemba 11, 2017 ikiwa ni kuenzi siku ya kisukari duniani
Novemba 14 ya kila mwaka.
"Kisukari
ni moja wapo ya magonjwa yasiyoambukiza na kwas asa huchangia asilimia mbili ya vifo vinavyosababishwa
na magonjwa hayo. Lakini ifikapo mwaka 2030 makadirio ni asilimia 7 ya vifo
nchini itatokana na kisukari "amesema.
Waane
amesema matembezi hayo yatahamasisha watu kupambana na ugonjwa huo hatari
duniani kwa kufanya mazoezi kama njia kuu ya kupambana na magonjwa
yasiyoambukiza.
Amesema
matembezi hayo yataanzia kiwanja cha mpira cha chuo cha Muhimbili (Muhas), kupitia barabara ya umoja wa mataifa kisha
kupita barabara ya Morogoro na Lumumba na kumaliza viwanja vya mnazi mmoja.
"
Mgeni rasmi atapata fursa a kuzungumzia ukubwa wa tatizo la kisukari nchini na
changamoto zinazowapata watu wenye kisukari nchini, "amesema.
Kauli
mbiu katika matembezi hayo ni 'Wanawake na kisukari, haki yetu kwa afya njema'.
No comments:
Post a Comment