Takwimu: Asilimia 17 watoto huzaliwa njiti...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu

TAKWIMU zinaonesha asilimia 13 hadi 17 ya watoto huzaliwa njiti  nchini.

Kaimu Mkurugenzi wa Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Janneth Mghamba akizungumza kwenye maadhimisho ya mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa Novemba 17 kila mwaka. Kushoto ni Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Hedwiga Swai.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Neema Rusibamayila wakati wa maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Watoto Njiti ambayo huadhimishwa Novemba 17 kila mwaka.

Amesema Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la vifo vya watoto wachanga walio chini ya mwezi mmoja hivyo kutokana na hali hiyo serikali inapaswa kudhibiti vifo kwa watoto wachanga.

“Serikali imeweka mikakati endeleveu  ya kupunguza vifo vya watoto njiti kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya afya nchini,”amesema.


Amesema moja ya program hizo ni kumsaidia mtoto kupumua baada ya kuzaliwa, kupanua huduma za watoto wachanga kwa kujenga wodi za watoto wachanga katika hospitali za manispaa na wilaya pamoja na kutoa mafunzo kwa wa hudumu wa afya jinsi ya ya kuhudumia watoto wachanga.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search