Waziri Mbarawa awataka wananchi kanda ya ziwa kujikomboa kiuchumi...soma habari kamili na Matukio...#share
Na
mwandishi wetu
WAZIRI
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewataka wakazi wa
kanda ya ziwa kutumia fursa ya uwepo wa uwanja wa ndege wa kisasa wa Geita
kukuza utalii, kilimo, ufugaji na biashara ya madini ili kuhuisha uchumi wa
mikoa ya kanda hiyo na kujikomboa
kiuchumi.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akipanda mti aina
ya Muashoki kama alama ya kumbukumbu ya sehemu iliyowekwa jiwe la msingi la
ujenzi wa Uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita, leo.
Amesema
hay oleo mkoani Geita alipokuwa akiweka
jiwe la msingi la uwanja huo katika kijiji cha Nyabilezi na amesisistiza
kila mwananchi kuangalia namna atakavyonufaika na uwanja huo.
“Serikali
imejipanga kuhakikisha kwamba usafiri wa anga unaimarika ili kurahisisha huduma
ya usafirishaji wa abiria, hivyo kuvutia watalii katika vivutio mbalimbali
nchini”, amesema Profesa Mbarawa.
Waziri
Mbarawa amesema katika kuhakikisha usafiri
wa anga nchini unaimarika Serikali
imekarabati Viwanja vya ndege vya Mpanda, Bukoba, Tabora na Mafia na ina
mpango wa kuvijenga kwa kiwango cha kisasa viwanja 11 nchini ili kuwezesha
ndege mpya za Shirika la Ndege (ATCL),
kutoa huduma katika mikoa mbalimbali.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale amesema
ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa mkoa wa Geita ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya
usafiri wa anga nchini ya mwaka 2003 inayooelekeza uwepo wa uwanja wa ndege wa
kisasa katika kila mkoa ili kurahisisha uchukuzi na kuchochea fursa za
kibiashara na kitalii katika maeneo mbalimabali ya nchi.
Mhandisi
Mfugale amesema Uwanja wa Ndege wa Geita ambao unajengwa na Kampuni ya
kikandarasi ya Mayanga ambayo ni ya mzawa kwa gharama ya zaidi ya bilioni 41.
“Uwanja
huu utakapokamilika utawezesha ndege kubwa aina ya Boeing 737 - 800 zenye uwezo
wa kubeba abiria 100 hadi 200 kuruka na
kutua, hivyo kuongeza na kurahisisha huduma ya usafiri wa anga katika Ukanda
huo”, amesema Mhandisi Mfugale.
Mkuu
wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Luhumbi, amesema wamejipanga kutumia uwanja
wa ndege wa Geita katika kukuza utalii na biashara mkoani humo na kuahidi
kuulinda uwanja huo na kutunza miundombinu yake.
Uwanja
wa Ndege wa Geita wenye urefu wa Kilometa 3 na upana wa Mita 45 unatazamiwa
kuwa na uwezo wa kuegesha ndege kubwa Tatu kwa wakati mmoja pindi
utakapokamilika.
No comments:
Post a Comment