400 wa chuo kikuu Dar es Salaam wajiunga CCM...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu
IKIWA ni muendelezo wa CCM kuvuna wanachama wapya, leo katika viwanja vya shule ya msingi kibangu wilayani Ubungo jijini Dar es Salaam takribani wanafunzi 400 wa shahada, stashahada na shahada za uzamivu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) wamejiunga na CCM.

Baadhi ya maafisa wa CCM kutoka makao makuu idara ya Itikadi na Uenezi, Shabani Shabani na Saidi Saidi 

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Itikadi na Uenezi wa CCM inasema katika mkutano wa ndani wa wanachama, uliyoratibiwa na viongozi wa Umoja wa Vijana Tawi la Mabibo, ulihudhuriwa na maafisa wa CCM kutoka makao makuu idara ya Itikadi na Uenezi, Shabani Shabani, Saidi Saidi na Debora Charles ambaye anatokea Idara  ya Siasa na uhusiano wa Kimataifa, viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM seneti ya Mkoa wa Dar es Salaam, Mwenyekiti wa serikali ya mtaa na wanachama. 

Mwenyekiti wa Tawi la Mabibo  Isack Ngombe  amesema wanafunzi wa UDSM "Wasomi kumuunga mkono rais Magufuli ni haki yao maana anafanyakazi nzuri, pia wanajiunga na CCM kwa kuwa ndio Chama pekee kinachoshughulika na shida za wananchi wanyonge".
Lakini pia amesema wapo wanafunzi wengi zaidi wa chuo kikuu wangependa kujiunga na CCM hivyo ni jambo la muda tu.

Maafisa kutoka makao makuu ya CCM wamewakaribisha wanachama wapya wa CCM na kuwaasa, kuwa wamechagua chaguo sahihi, wawe wanachama waaminifu wanaosadifu CCM MPYA na TanzaniaMpya kwa kujitoa kusoma kwa bidii, kushirikiana na wenzao, kuwa mstari wa mbele kutimiza wajibu wao na kutetea rasilimali za taifa letu.


Tangu kutangazwa mageuzi makubwa kwa vitendo  ndani ya CCM na serikali yake wananchi wamakundi mbalimbali wamekuwa wakijiunga na CCM kwa wingi wakiamini "CCM  ni chama cha siasa imara na ni daraja la kuwaunganisha watu na serikali walioichagua na kuiunganisha serikali na watu inayotaka kuwahudumia."

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search