CCM yaonya.....soma habari kamili na matukio360...#share



Na Mwandishi Wetu
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimewaonya wanachama na viongozi wakati huu wa uchaguzi unaoendelea ndani ya chama katika ngazi ya mkoa na Jumuia zake kutojihusisha na vitendo vya rushwa.

Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni rais wa Tanzania, Dk John Magufuli.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole imebaini kuwepo kwa minong'ono na tetesi za vitendo vya rushwa katika baadhi ya mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa chaguzi za Mwenyekiti, Mwenezi wa NEC na wote wanaoomba dhamana za uongozi katika jumuiya za chama. umoja wa vijana (UVCCM), umoja wa wanawake (UWT), na jumuiya ya wazazi (WAZAZI).

"Vitendo hivi havikubaliki, havivumiliki,na nikinyume na misingi, maadili na miiko ya Chama cha Mapinduzi ," imesema.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search