Mbeya kwanza yaacha wachezaji saba...soma habari kamili na matukio360...#share


Yusta Nkwelengushe,Mbeya

MABOSI  wa klabu ya Mbeya kwanza ya jijini hapa  umeamua kuachana na wachezaji saba walioitumikia timu katika mzunguko wa kwanza wa ligi daraja la kwanza  kwa makosa ya utovu wa nidhamu pamoja na kushuka kiwango.

Timu ya soka ya Mbeya kwanza

Kocha mkuu wa timu hiyo inayoshiriki ligi daraja la kwanza , Maka Mwalwisi amesema wachezaji hao walioachwa ni wale waliokuwa hawaonyeshi juhudi za kuipigania timu  ipate mafanikio na kusonga mbele.

Amesema wachezaji wengi walioachwa ni wale  waliosajiliwa kutoka mkoani Pwani na sasa kikosi kinabaki na wachezaji 22 waliokuwepo tangu mwanzo wa msimu huu wa ligi .

Mwalwisi amesema ‘‘Nilijaribu kukaa nao ili wajirekebishe lakini hilo lilishindikana na wale ambao viwango vilionekana kushuka nilikuwa namfanyisha  mazoezi  mmoja baada ya mwingine nao nikaona ni mzigo tu.’’

Amesema wachezaji hao walioachwa pia walitaka kukwamisha safari yao ya kuipigania timu ili iweze kupanda daraja kutoka Ligi daraja la kwanza hadi kushiriki  Ligi Kuu msimu ujao.

Baada ya kutoa taarifa kwa Mkurugenzi wa timu Batchu Shiraz naye aliridhia na kuwaandikia barua za kuachana na timu yetu ili tupate nafasi ya kuongeza wengine wazuri watakaoisaidia timu.

Katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo,Mbeya kwanza imejipanga kuongeza nafasi za wachezaji wanne pekee ili kukamilisha kikosi cha wachezaji 26 watakaoitumikia timu hiyo.

Nafasi wanazotarajia kusajili ni washambuliaji watatu pamoja na kiungo  ambao wataungana na wenzao ili kuhakikisha timu inafanya vyema katika mechi zake tano ilizobakiwa nazo.
 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search