Hivi hapa viwango vipya vya soka Duniani...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mashirika ya kimataifa
Shirikisho la soka Ulimwenguni FIFA limetoa viwango vipya vya soka duniani ambapo Tanzania imeshuka kwa nafasi tano  kutoka  120 hadi 125

Kikosi cha timu ya soka ya Ujerumani

Katika orodha hiyo sasa  Ujerumani wamerudi tena kuchukua nafasi yao ya kwanza ambayo hapo mwanzo ilienda kwa timu ya Brazil.

Brazil waliokuwa wakishika nafasi ya kwanza sasa wamekuwa nafasi ya pili huku Ureno waliokuwa nafasi ya sita sasa wako nafasi ya 3 na Argentina waliokuwa nafasi ya 3 wameshuka hadi 4. Waliokuwa nafasi ya 3 wameshuka hadi 4.

Ubelgiji wamepanda hadi nafasi ya 5 kutoka 9 walipokuwa huku nafasi ya 6 ikienda kwa Poland, timu ya taifa ya Swiztrland wako katika nafasi ya 7 huku ya 8 ikikamatwa na Ufaransa.

Mabingwa wa Amerika Kusini timu ya taifa ya Chile wako nafasi ya 9 huku wanaofunga orodha ya 10 bora ni timu ya taifa kutoka bara la America timu ya Colombia.

Timu ya taifa ya Uingereza ambayo imeshuka hadi nafasi ya 15 ikiwa ni baada ya miaka 17 kufika katika hatua hiyo na wakipitwa na  Wales walioko 13.

Kwa upande wa kumi bora ya Africa, Misri wanaongoza wakifuatiwa na Tunisia huku Wasenegal wakiwa katika nafasi ya 3, ya 4 ikienda kwa DRC.


Nigeria wako nafasi ya 5, wakifuatiwa na mabingwa wa Africa timu ya taifa ya Cameroon huku Burkina Fasso wakishika namba 7, 8 ni Ghana, 9 Ivory Coast na 10 ni Morocco.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search