Kinana akubali yaishe CCM...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana amekubali ombi la Rais John Magufuli  ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho la kumtaka kuendelea kumsaidia kwa nafasi hiyo.
Katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.

Rais Magufuli ametoa ombi hilo akifungua mkutano mkuu wa CCM taifa unaoendelea mjini Dodoma.

“Ni mshukuru mzee Kinana kwa kunisaidia sana katika kukiongoza chama hiki na nimategemeo yangu ataendelea kunisaidia pia hapo baadae,” amesema Rais Magufuli.

Awali kulikuwa na minong’ono kuwa katika mkutano huu angetangazwa katibu mkuu mwingine lakini kwa hatua hiyo ni kwamba inamaliza uvumi huo.

Akiwasilisha agenda za mkutano huo Kinana amesema anakubali ombi la mwenyekiti wake kwani kauli yake ni amri.

“Nashukuru kwa kuendelea kuniamini, tumekuwa tukiongea mara nyingi mambo ya chama na yangu binafsi, lakini napogusia masuala yangu binafsi amekuwa akisema nisubiri na kuniuliza nawasiwasi gani,” amesema Kinana.


Katibu mkuu huyo amemuahidi Rais Magufuli kuendelea kumsaidia kazi hiyo ya kuleta mabadiliko katika chama kwa ufanisi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search