Magufuli atoa msimamo wake...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es salaam

MWENYEKITI wa CCM, John Magufuli ametoa msimamo wake wa kiutendaji kwa kipindi cha miaka mitano ijayo 2017-2022.
Mwenyekiti wa CCM, John Magufuli

Amesema mtendaji yoyote atayekwenda kinyume atashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu na  kanuni za chama hicho.

Msimamo huo ameutoa leo mjini Dodoma alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa CCM na kwamba mambo makuu manne ndio msingi na dira ya utendaji katika chama hicho.

Magufuli ambaye pia ni rais ameyataja mambo hayo kuwa ni kuimarisha CCM kwa kuongeza idadi ya wanachama wa uhakika.

Kuhakikisha chama kinajitegemea kiuchumi na  ni aibu kwa chama kuwa tegemezi.

 Viongozi wa CCM kuwa kiungo kati ya wananchi na serikali.

“Na ya nne ni  viongozi kuwa waadilifu na mfano kwa wananchi,” amesema Magufuli na kuongeza  “Mkutano huu ukiridhia ndio malengo makuu  ya mradi wa awamu ya nne ya kujenga na kukiimarisha chama chetu.”







About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search