Kocha Hemed Moroko ataka Zanzibar Heroes isivunjwe...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwajuma Juma, Zanzibar
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’ Hemed Moroko ametakatimu hiyo isivunjwe,  iendelezwe na kwamba itakuwa timu bora katika mashindano yajayo.


Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud akimvisha shada la maua kocha mkuu wa Zanzibar Heroes, Hemed Moroko mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Zanzibar na Timu yake ikitokea Kenya Katika mashindano ya CECAFA CHALLENGE CUP.

“Kama ambavyo nilivyosema mwanzo, kuwa timu hii unaweza kuiona ni ndogo lakini kwa sasa sio ndogo, lakini changamoto wahusika wameweza kuziona na mimi katika ripoti yangu naweza kutoa ripoti kuwa iendelee kuwepo kwa kufanya mazoezi kila baada ya muda”, amesema Moroko

Ameyasema hayo mara  baada ya  kuwasili visiwani Zanzibar wakitokea nchini Kenya.

Moroko amesema licha ya changamoto walizopata wakati wa kuiandaa timu hiyo walipofika huko walitulia na kutafuta njia ya kuweza kujipanga ili waweze kufanya vizuri katika michuano hiyo.

“Kulikuwa na changamoto wakati tulipoondoka hadi tulipofika lakini zilipunguwa na kuweza kujipanga vizuri hadi kufikia hatua hii ya fainali”, alisema Moroko.

Nao wachezaji  wa timu hiyo wamesema  mashindano
yalikuwa magumu.

Mlinzi wa timu hiyo Issa Haidar Mwalala amesema haikuwa kazi rahisi kufikia hatua ya fainali kwa kuwa mashindano hayo yalijaa wachezaji bora kutoka timu nyingine.

“Sisi hatukuwa na wachezaji professional kama walivyo wenzetu lakini tulifanyakazi kubwa hadi kufikia hatua hii”, amesema.

Ametaja sababu ya umoja, ushirikiano na nidhamu kuwa uliwapa nguvu hadi kufikia hatua waliyofikia.


Pia  siri  nyingine ya mafanikio hadi timu kufikia hatua ya fainali ni kujipanga na kutulia wakati wanapocheza mpira.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search