Kesi mhasibu Takukuru upelelezi haujakamilika...soma habari kamili na matukio360..#share
Na Abdulrahim Sadiki, Dar es salaam
UPANDE wa jamhuri katika
kesi inayomkabili Mhasibu Mkuu wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Godfrey Gugai anayedaiwa
kuwa na utajiri wa kutisha kwa kumiliki
mali zenye thamani ya bilioni tatu ambazo haziendani na kipato chake, umedai
upelelezi haujakamilika.
Wakili wa Serikali Mkuu,
Vitalis Peter amedai hayo leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya
Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati shauri hilo linalomkabili Gugai na
wenzake watatu lilipopelekwa kwa kutajwa.
Kutokana na kutokamilika kwa
upelelezi huo, Wakili Peter ameomba shauri hilo kuahirishwa hadi tarehe
nyingine kwa kutajwa.
Hata hivyo, Wakili wa
utetezi, Alex Mgongolwa aliomba upande wa jamhuri watoe maelezo ambayo
yataeleza lini upelelezi utakamilika ambapo upande wao utajua siku ya kuanza
kwa usikilizwaji wa shauri hilo.
Akijibu hoja hiyo, Wakili wa
Serikali Peter alidai kukamilika kwa upelelezi ni hatua, hivyo hawawezi kueleza
kwa asilimia ngapi ila bado unaendelea na wako katika hatua nzuri.
Wakili huyo alidai tareje
ijayo wataeleza hatua ya upelelezi ilipofikiwa. Baada ya kusikiliza hoja za
pande zote husika, Hakimu Simba aliahirisha shauri hilo hadi Januari 2, mwakani
kwa kutajwa na washitakiwa walirudishwa mahabusu.
Mbali na Gugai, washitakiwa
wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera
Washitakiwa hao
wanaokabiliwa na mashitaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu,
kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya
viwanja katika maeneo mbalimbali.
Gugai na wenzake wanasota
mahabusu kutokana na kukabiliwa na mashitaka ya utakatishaji fedha ambayo
hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.
Katika mashitaka hayo,
shitaka la kwanza ni la kumiliki mali ambazo hazina maelezo ambalo linamkabili
Gugai anayedaiwa kati ya Januari 2005 na
Desemba 2015, mkoa wa Dar es Salaam, akiwa ofisa wa umma ameajiriwa na TAKUKURU
anamiliki mali zenye thamani ya sh. 3,634,961,105.02 ambazo haziendani na
kipato chake cha sasa wala cha nyuma cha sh. 852,183,160.46 na alipotakiwa
kutoa maelezo alishindwa kuyatoa juu ya mali hizo zilizoko kwenye umiliki wake.
No comments:
Post a Comment