ACT Wazalendo: Hatuungi mkono mgombea yeyote ubunge, udiwani...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimesema hakitaunga mkono mgombea wa chama chochote katika uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani unaotarajiwa kufanyika Februari 17, 2018.
Wakwanza Kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo Addo Shaibu akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani na wakwanza kulia ni Naibu Katibu mkuu wa chama hicho Bara Msafiri Mtemelwa.

Msimamo huo umetolewa  jijini Dar es Salaam na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Addo Shaibu katika mahojiano maalum na matukio360, amesema hatua ya kuunga mkono itakuwa ni kuridhia ukiukwaji wa kanuni na taratibu za uchaguzi unaofanywa na NEC na serikali.

“Kusimama na kuunga mkono mgombea wa chama fulani ni sawa na kuunga mkono ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi unaofanywa na NEC na vyombo vya dola, kwa hiyo msimamo wetu hatutajihusisha kwa namna yoyote ile,” amesema Shaibu.

Shaibu amesema kuwa wangetamani wagombea wa vyama vya upinzani washinde lakini wanaamini kwa jinsi hali ilivyo hawatashinda katika uchaguzi huu.

Amebainisha kuwa chama kitaungana na vyama vingine vya upinzani katika kupigania masuala ya kidemokrasia tu na si kwenye kusimamisha wagombea.

Awali Naibu Katibu Mkuu Bara wa chama hicho Msafiri Mtemelwa akitoa msimamo wa chama mbele ya waandishi wa habari juu ya ushiriki katika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Siha na Kinondoni  amesema hakitashiriki.

“Tunapenda kuweka bayana kwamba chama chetu hakitoshiriki kwenye uchaguzi wa marudio wa Februari 17, 2018 kwenye jimbo la Kinondoi na Siha na udiwani kwenye kata tisa,” amesema Mtemelwa.

Amefafanua kuwa msimamo huo unatokana na ukweli kwamba sababu zilizolalamikiwa kwenye uchaguzi wa Januari 13, 2018 hazijabadilika kwa sehemu kubwa.

Amemeleza mageuzi madogo yaliyofanywa na Tume ni kauli yao ya kuwataka wakuu wa wilaya kuacha kuingilia uchaguzi jambo ambalo ni dogo katika malalamiko ya vyama vya upinzani.

Mtemelwa amesema chama kimeona kuna umuhimu kwa vyama vya upinzani kuendelea kuikabili NEC na vyombo vya dola kwa pamoja na kwaba kitaendelea kushinikiza mabadiliko muhimu kutokea ili chaguzi ziwe huru na haki.

Pia amesema kitaendelea kushirikiana na vyama vya upinzani na wadau  wengine wa kidemokrasia kwenye mikakati ya kushinikiza Tume na serikali kufanya mageuzi ya mchakato wa uchaguzi.

Vyama vikuu vilivyosimamisha wagombea katika majimbo mawili ya Siha na Kinondoni ni CCM, CUF  ya Lipumba na Chadema kwa mwamvuli wa Ukawa.

Kinondoni Wagombea ni Maulid Mtulia (CCM), Rajab Juma (CUF Lipumba), Salum Mwalimu (Chadema) na Siha wagombea ni Elvis Christopher Mosi (Chadema), Dk. Godwin Mollel (CCM).

Kwa mujibu wa Ofisa habari wa CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba, Abdul Kambaya akizungumza na matukio360 amesema hadi sasa hawajapewa jina la mgombea katika jimbo la Siha hivyo wanasubiri watumiwe ndipo watakapoliweka hadharani.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search