Magufuli, Dk Shein, Mangula wachaguliwa tena...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
MKUTANO wa halmashauri kuu ya  CCM(NEC) leo imemteua rais John Magufuli kugombea nafasi ya mwenyekiti wa chama  hicho taifa,  Dk Shein makamu mwenyekiti  Zanzibar na Mangula Makamu Mwenyekiti  Bara.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho Humphrey Polepole  kikao hicho kimefikia uamuzi huo baada ya kutafakari kwa kina na kwa kuzingatia mwelekeo mpya wa CCM. Awali kabla ya Nec. Kikao cha kamati kuu(CC) kilitangulia.


Pia amesema mkutano  mkuu wa CCM utafanyika  Desemba 18 na 19, 2017 ili kuwapitisha viongozi hao rasmi watakaongoza hadi mwaka 2022.






About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search