Sintofahamu yatawala Takukuru kumkamata Mchechu wa NHC...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Dar es
Salaam
TAARIFA zilizosambaa kuanzia
mchana wa hii leo Jumapili ni kwamba
aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la nyumba(NHC) kabla ya kusimamishwa hapo
jana, Nehemiah Mchechu amekamatwa na TAKUKURU kwa mahojiano.
Nehemiah Mchechu
Taarifa hizo zinadai Jumanne ijayo atafikishwa mahakamani kujibu makosa ya Uhujumu Uchumi, Uchepushaji
na matumizi mabaya ya madaraka.
Hata hivyo ili kuthibitisha taarifa hizo matukio360
aliwatafuta baadhi ya watendaji wa Takukuru akiwamo mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Valentino Mlowola ambaye amesema ; "Siwezi kuzungumza chochote mtafute msemaji wa
Takukuru, Pia kumbuka leo ni Jumapili nipo katika ibada hivyo sipo katika
nafasi nzuri ya kuzunguma hayo labda kesho Jumatatu.’’
Matukio360 ilipomtafuta Tunu
Mleli ambaye andiye anayefahamika kama msemaji wa Takukuru alijibu ; "Samahani mtafute msemaji wa Takukuru na kutoa namba za huyo aliyedai kuwa
msemaji. Pia namba hizo zilipopigwa hazikupatikana.’’
Jana waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William
Lukuvi alitangaza kumsimamisha Mchechu kwa madai ya matumizi mabaya ya fedha na
ofisi.
No comments:
Post a Comment