Magufuli : NHC ijitathimini, inamadudu...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
RAIS John Magufuli amelitaka shirika la nyumba(NHC)  kujitathimini kutokana na matumizi yake ya kifedha na kwamba inamadudu.

Pia ametishia kuivunja bodi ya shirika hilo kama itaendelea na misuguano ya chini kwa chini.

Rais John Magufuli

Ametoa agizo hilo leo mjini Dodoma alipokuwa akifungua nyumba za makazi za Iyumbu Dodoma na kwamba serikali itakuwa tayari kuizamini NHC kukopa fedha  bilioni 200  kuendeleza miradi nchini.

Amesema watendaji wa NHC wanamisuguano ya ndani kwa maslahi binafsi ikiwamo kutaka nafasi ya mtendaji mkuu wa shirika hilo, Nehemia Mchechu na kuwa mingine inachochewa na wanasiasa.

‘’Waziri wa ardhi, bodi ya NHC na wakurugenzi mkae na kujitathimini kuhusu mwenendo mzima wa matumizi ya fedha za NHC. Mkirekebisha hilo nitakuwa  tayari kusaini na kulizamini shirika kukopa fedha kuendeleza miradi mbalimbali,’’ amesema Magufuli.

Rais Magufuli amesema pamoja na kazi nzuri inayofanywa na NHC lakini bado kuna  ‘madudu’ matumizi mabaya ya kifedha katika baadhi ya miradi na kuuelezea mradi wa Kawe jijini Dar es salaam.

‘’Mradi wa Kawe jijini Dar es Salaam una ‘madudu’ najua mradi unaubia na mwekezaji wa nusu kwa nusu, mtu mwenyewe namjua. Ukikamilika anaweza kudai fidia yoyote, anaweza hata kwenda mahakamani,’’ amesema

Amesema ni vigumu kwake kusaini fedha wa watanzania kwa ajili ya matumizi mabovu.

Amesema hivi karibuni amelipa shirika hilo zaidi ya bilioni 3.8863 kwa ajili ya ununuzi wa nyumba za wafanyakazi wa serikali na kwamba zitumike kuendeleza na kuboresha makazi nchini.

Mradi huo wa Iyumbu hadi leo takribani nyumba 150,000 zimekamilika na utakuwa na nyumba 300,000

Awali waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema NHC inatarajia kujenga kiwanda cha kuzalisha bati.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search