Mwakyembe atoa msimamo kwa vilabu vya soka....soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI imevitaka vilabu vya mpira wa miguu nchini vilivyoanzishwa kwa mfumo wa wananchama vinavyotaka kubadili mfumo wa kiuenedeshaji wa hisa kutenga asilimia 51 kwa ajili ya wananchama na 49 kwa ajili ya mnunuzi.
Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo imekuja ikiwa hivi karibuni klabu ya Simba ilifanya mabadiliko ya umiliki wa timu kuwa katika mfumo wa hisa na bilionea Mohammed Dewji akishinda uwekezaji wa klabu hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Dk. Harrison Mwakyembe  amesema lengo ni kulida asili na historia ya vilabu husika.

“Haya ni matakwa ya kanuni za sheria la baraza la michezo la taifa (BMT) (marekebisho) ya mwaka 2017 ambazo zinasomwa kwa moja na kanuni za sheria za BMT za mwaka 1999, ambazo katika kanuni hizo zitaitwa kanuni kuu,” amesema Dk. Mwakyembe.

Ufafanuzi wa kanuni

Kanuni kuu zinarekebishwa kwa kuongeza mara baada ya kanuni ya 18, kanuni mpya ya 18A kama ifuatavyo..

Uuzwaji wa hisa vilabu vya michezo katika kanuni ya 18A,-(1) Vyama au vilabu vya michezo  vilivyoanzishwa na wanachama vikiamua kuuza hisa zake vinapaswa kutenga asilimia 51 kwa ajili ya wananchama wake na asilimia 49 kwa wanaotaka kununua.

(2) Katika kusimamia utekelezaji wa kifungu cha (1) cha kanuni hii, chama cha kitaifa kinachosimamia mchezo husika kinapaswa kutengeneza mwongozo wa muundo wa vilabu hivyo kwa mtindo wa hisa.

(3) Maombi ya uuzaji wa ununuzi wa hisa yatalazimika yaidhinishwe na chombo husika kinachosimamia mitaji na dhamana kwa mujibu wa sheria za nchi.

(4) Wakati wa kuuza hisa, vyama au vilabu vya michezo vilivyoanzishwa na wanachama vitalazimika kuwa na azimio na kwamba watakaoruhusiwa kununua hisa ni wanachama waliohakikiwa na klabu husika kupitia taratibu zilizowekwa kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na uwazi.


Waziri Mwakyembe amesisitiza kuwa lengo lakuzungumzia suala hilo si kwa ajili ya klabu ya Simba na Mohammed Dewji kwa kufanya mabadiliko ya kimfumo lakini ametaka kuzingatiwa kwa kanuni na taratibu za nchi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search