Makalla akabidhi mabati 154, mifuko ya saruji 100....soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Mbeya
SERIKALI mkoani Mbeya imetoa msaada wa mabati 154 na mifuko 100 ya saruji yenye thamani ya   milioni 4 katika  zahanati ya kata ya  Mwasanga na ujenzi wa kituo cha afya Iduda.


Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla (kushoto) akikabidhi mabati na mifuko ya seruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na kituo cha afya mkoani humo

Akikabidhi msaada huo leo mkuu wa mkoa huo, Amos Makalla amesema mpango mkakati wa serikali ya mkoa ni kuchangia vituo vya afya na zahanati zilizojengwa kwa nguvu ya wananchi.

Pia wakati ujenzi huo ukiendelea ameagiza  uongozi wa halmashauri ya jiji  kuboresha miundombinu ya barabara.


"Huu ni mpango mkakati wa mkoa katika kuchangia kila kata na  kijiji ambavyo vimethubutu kujenga vituo vya afya na zahanati na sitoishia hapo nitahahakisha pindi vinapokamilika kunakuwepo na  madaktari na wauguzi,"amesema.


Makalla amesema Serikali ya viwanda haitoweze kufanikiwa ikiwa wananchi wanakosa huduma za msingi za maji, miundombinu  ya barabara na huduma za afya  hususan kwa wanaoishi  pembezoni mwa mji.

Ameonya watendaji na wanasiasa kutoingiza maslahi binafsi katika msaada huo na ametaka  wananchi washirikishwe katika kila hatua ili kuondoa malalamiko yanayoweza kujitokeza katika miradi hiyo.
Diwani wa kata Mwasanga, Joe Hokola amesema  wananchi wamechangia  milioni 1.2 za ununuzi wa vifaa mbalimbali katika zahanati.


Mkazi wa Mwasanga, Sophia Mumbonege amesema ujenzi wa kituo hicho cha afya na zahanati kitawezesha upatikanaji wa huduma bora za afya  kwa kupunguza msongamano   katika  Hospitali ya mkoa wa Mbeya

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search