Ukawa ‘kususia’ uchaguzi wa ubunge, udiwani....soma habari kamili na matukio360..#share


Na mwandishi wetu, Dar es Salaam
VYAMA vya siasa vinavyounda umoja wa katiba(Ukawa) vimetaka uchaguzi wa marudio wa ubunge na udiwani wa Januari 13, 2018 uahirishwe kwa kuwa mazingira ya uchaguzi hayako sawa.

Pia vimesema kama Serikali na  Tume ya Uchaguzi (Nec) itashindwa kutekeleza hilo, havitoshiriki katika uchaguzi huo.

Freeman Mbowe

Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na viongozi wa Ukawa walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari.

Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe amesema Nec ilipaswa ikae na wadau na vyama vya siasa kujadili utaratibu mzima wa jinsi uchaguzi huo utakavyofanyika.

‘’Lakini tumeshtuka kuona Nec inatangaza ratiba ya uchaguzi wa majimbo na kata pamoja na sheria kuwaelekeza hivyo lakini kutoka na kutokuwepo kwa mazingira sawa na ukiukwaji wa haki na sheria katika uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani,mazingira ya kufanyika uchaguzi mwingine hayako sawa. Hivyo tunaiomba NEC na Serikali kuahirisha uchaguzi huu na wakishindwa kufanya hivyo Ukawa hatutoshiriki uchaguzi huo.’’ amesema Mbowe

Akitolea mfano amesema jimbo la  Longido Kaskazi halipo wazi  na kuwa kuna rufaa  imekatwa  katika mahakama ya rufani na  wameijulisha tume lakini bado  haijawajibu

Wametaka Nec ikae na wadau wake ikiwamo vyama vya siasa kujadili suala hilo na kwamba uchaguzi si mapambano na ni lazima ufuate taratibu, sheria na kanuni za uchaguzi  .

‘’Kuna viashira vya kupoteza amani ya nchi, upo ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu’’ amesema Mbowe

Kuhusu kwenda mahakama wanaamini kuwa wakati mwingine inachelewesha haki ya msingi  na kwamba haki nyingine zinapatikana kwa kujadiliana nje ya mahakama.

Jimbo la Singida Kaskazini, Longido Kaskazini na Songea Mjini ndio majimbo yaliyotangazwa na Nec kurudia uchaguzi Januari 13, 2018



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search