Makamba: Viongozi muwe na maarifa.....soma habari kamili na matukio360..#share


Na Salha Mohamed, Dar es Salaam

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira,  January Makamba amewashauri viongozi  nchini kuwa na maarifa  na kwamba uongozi si cheo bali ni mamlaka. 

Waziri wa nchi, ofisi ya makamu wa rais, muungano na mazingira,  January Makamba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya uongozi na maadili kwa wanafunzi viongozi wa vyuo vya elimu ya juu nchini yaliyoandaliwa na Shirikisho la wanafunzi wa elimu ya juu (TAHLISO), ili kuwajengea uwezo wa uongozi. 

Amesema kiongozi si cheo bali ni mamlaka kwani unaweza kuwa na cheo na usiwe na mamlaka kwa unaowaongoza. 

"Unakuwa na cheo lakini kuna kufuatwa na kutiiwa na ili uwe na manufaa kwa watu lazima uweze na uwe na maarifa ya kusaidia watu na kuwashirikisha katika mambo yanayowahusu," amesema. 

Amesema kiongozi anapaswa kuishi kwa mfano na tabia njema na si uwezo wa kusherehesha watu jukwaani.

Amesema lazima nchi iwe na utaratibu wa kuandaa na kuwajengea uwezo na maarifa viongozi katika vyuo vyao huku akibainisha mambo yasiyitakiwa kama ulevi, usinzi, dawa za kulevya, uasherati, chuki, ukabila hapaswi kuwa navyo.  

"Tunafarijika katika mafunzo haya kuna mada mbalimbali ikiwemo maadili ya uongozi, kupambana na dawa za kulevya,miiko ya rushwa, kujitambua na mazingira ya uongozi.

"Vijana hawa wakijengwa kwenye maadili, taifa litapata viongozi wazuri, "amesema. 

Kwa upande wake, Katibu Sekretarieti ya maadili, Idara ya Viongozi wa siasa,  Waziri Kipacha amesema wameanzisha klabu za maadili kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo. 

"Mafunzo haya ni sehemu ya jukumu la sekretarieti ya maadili katika kukuza na kujenga uadilifu kwa vijana ngazi za shule,"amesema. 

Amesema mafunzo hayo yatawaandaa wanafunzi hao kujua maadili ambayo kiongozi wa umma anapaswa kuwa nayo pindi anapoteuliwa


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search