Maombi ya CUF Lipumba kumkataa jaji yatupwa...soma habari kamili na matukio360..#share


Na mwandishi wetu, Dar es Salaam
MAHAKAMA kuu jijini Dar es Salaa leo imetupilia mbali maombi ya kumtaka Jaji Wilfred Ndyansobera ajitoe kusikiliza mashauri ya CUF yanayoendelea katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam

Profesa Ibrahim Lipumba

Maombi hayo yaliwasilishwa mahakamani hapo na watu 10 wanaodaiwa kuwa ni wajumbe wa Bodi ya Wadhamini CUF ya Mwenyekiti anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba, ambapo barua ya maombi hayo ilikuwa na malalamiko sita ikiwemo wadaiwa kutokuwa na imani na jaji.

Akisoma maamuzi ya kutokujitoa kusikiliza mashauri hayo leo  mbele ya mahakama, Jaji Ndyansobera, amedai kuwa baada ya kuchunguza malalamiko hayo, na kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili, amegundua kuwa hakuna kitu kinachoonyesha kama anapendelea upande mmoja, pia malalamiko hayo yalikuwa si sahihi kisheria kutokana kwamba watu 10 waliowasilisha maombi hayo, ni watu binafsi na si bodi halali ya wadhamini ya CUF.

“Bodi ya CUF ina taratibu zake za kutekeleza majukumu yake, mtu hawezi kusema anatumwa na bodi, bali bodi hufanya kazi zake. Jaji kujiondoa sio kitu chepesi ni kitu kizito,” amesema.

Jaji Ndyansobera amedai kuwa, katika kusikiliza mashauri ya CUF, alifuata sheria na katiba ya nchi, ambapo sheria inamtaka jaji kutekeleza majukumu yake katika kutoa haki, bila ya woga wala upendeleo au shinikizo kutoka upande wowote.

“Kuna mambo mawili ya msingi ya kuzingatia, jaji anatakiwa kujiondoa kwa kuzingatia mazingira ya kesi kama alikuwa anapendelea… pili kama kuna uhusiano wa karibu na mtu mmojawapo kwenye kesi au masilahi binafsi, jaji inatakiwa ujiondoe. Mahakama inatakiwa kuwa huru, jaji au Mahakama inaweza kuamua kesi kwa kuzingatia ushahidi ulioko mbele yake pasipo kupata mashinikizo kutoka nje na ubaguzi,” amesema.


Hali kadhalika ametaja sababu tano zilizopelekea kutokujitoa katika kusikiliza mashauri hayo, ikiwemo kuzuia ucheleweshwaji wa kesi, upotevu wa fedha, pia Jaji aliyekuwepo (Ndyansobera) ameshatoa maamuzi kwenye baadhi ya kesi hivyo inabidi aendelee kusikiliza mashauri kutokana kwamba anazijua kesi vizuri.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search