Makonda atoa runinga 69 kwa Magereza na Hospitali...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu
Mkoa wa Dar es Salaam umeadhimisha *Siku ya Uhuru kwa Kuwatembelea Wafungwa na Maabusu* kisha kupata *Chakula cha Pamoja* na kutoa huduma ya *Masaada wa Kisheria na Ushauri na Saha* kwa Wafungwa na Mahabusu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Katika Maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam *Mhe. PAUL MAKONDA* ametoa Msaada wa *Runinga za Kisasa 69* (Flat Screen) *Touch* zenye ukubwa wa *Inch 40* kwa *Magereza na Hospital* zote za Dar es Salaam *kuwezesha Wafungwa na Wagonjwa kupata haki ya kikatiba ya kupata Habari.*
*Hii ni Historia kwa Dar es salaam kuwa Mkoa wa kipekee wenye Runinga Magerezani* zinazowawezesha Wafungwa na Mahabusu kupata *Habari na Hotuba za Rais* ili kuwapunguzia *Msongo wa Mawazo* ili wasiwe na Mawazo ya kujiua ambapo zitagawanywa kwenye Magereza ya *Segerea, Keko na Ukonga*.
*RC MAKONDA* aliongozana na *Viongozi wa Dini* waliowafariji Wafungwa na Kuwafanyia *Sala na Dua* huku Watu wa *Ustawi wa Jamii* wakitoa Msaada wa *Ushau na Saha* kwa Wafungwa.
*MAKONDA* ambae *amepokelewa kwa Furaha kubwa*na Wafungwa wa Gereza hilo amewasihi *kutokata Tamaa* kwakuwa bado wanayo nafasi ya *kutimiza ndoto zao baada ya kumaliza kifungo* ambapo amewahimiza kuwa *Mabalozi Wazuri kwa Jamii.*
Ili kupunguza msongamano wa Mahabusu Gerezani *RC MAKONDA* amesaidia zaidi ya Mahabusu na Wafungwa *200* wa Gereza la Segerea kupata *Msaada wa Sheria* ambao walikuwa hawana uwezo kifedha.
Aidha *MAKONDA* ametoa *Magodoro 100, Vifaa vya Usafi na Sabuni za Kuoga na Kufua* kwa Wafungwa na Mahabusu.
Baadhi ya Maabusu na Wafungwa wamemshukuru *RC MAKONDA* kwa kuwa *kiongozi wa Kwanza na wa pekee* aliewatembelea na *kupata chakula cha pamoja, kuwapatia Runinga, kusikiliza changamoto zao na kuwapatia Wanasheria na watu wa Ustawi wa Jamii* kitendo kilichowafariji.
Aidha Wameshukuru pia kitendo cha *RC MAKONDA* kusikiliza Changamoto zao na kuzipatia majibu ambapo *wamemuahidi kuwa wamebadilika na watakuwa mabalozi wazuri kuhimiza jamii kuzingatia Sheria.*
About Author Matukio360
Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.
No comments:
Post a Comment