Mbunge akanusha kuhamia CCM....soma habari kamili na matukio360..#share
Na Abraham Ntambara,Dar es salaam
MBUNGE wa Moshi Vijini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema)
Antony Komu amesema hawezi kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi
(CCM).
Mbunge wa Moshi Vijijini Antony Komu, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja baada ya siku kadhaa kuwepo kwa uvumi kuwa
yeye ni mmoja wa wabunge wa Chadema ambao wangetarajiwa kukihama hivyo taarifa
hii inahitimisha uvumi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
waziri huyo kivuli wa viwanda, biashara na uwekezaji , amesema atakuwa ni mtu
wa ajabu kuhamia CCM na kuiunga mkono serikali ambayo inavunja katiba ya nchi.
“Nitakuwa ni mtu wa ajabu sana kuungana na serikali hii, kwa
mtu mwenye akili timamu huwezi kuwa sehemu ya serikali hii ambayo inaminya
uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa siasa, tulikuwa na bunge ‘live’ lakini hii
fursa imeondoshwa,” amesema Komu.
Komu amesema kuwa hajawahi kusikia wala kutumiwa ujumbe wa
simu kushawishiwa kujiunga na CCM na ni kutokana na kwamba yeye hawezi
kujaribiwa katika hilo hilo na kuingia katika mtego huo.
Amedai kuwa uvumi dhidi yake huenda kuwa ni propaganda
zinazofanywa na chama tawala ili kuhamisha mijadala ya msingi katika nchi kama
ya hali ya kudorola kwa uchumi hivyo serikali kutumia mwanya huo kukwepa kujibu
mijadala hiyo.
Amesema kuwa yeye ni mmoja wa waanzilishi wa mfumo wa vyama
vingi hivyo ataonekana mtu wa ajabu kuhama chama kwani vyama vya upinzani
vinahitajika ili kuikosoa serikali inapokosea ili mambo mengine yaende vizuri.
Kwa upande mwingine Komu amesema kuwa wanaohamia CCM wamekuwa
wakitoa hoja dhaifu ambazo haziwezi kumsawishi mtu mwenye kujielewa.
Amesema wapo wanaohama vyama vyao kutokana na serikali
kuwasumbua katika shughuli zao pamoja na kuwapa vitisho mbalimbali.
Pia amedai kuwa wanaohama ni wale waliochoka kutokana na
madeni mbalimbali hivyo wanarubuniwa ili kuweza kupatiwa msaada wa madeni yao.
No comments:
Post a Comment