Mbunge Lijualikali, Suzan Kiwanga mambo magumu....soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MBUNGE Peter Lijualikali wa Kilombero na Suzan Kiwanga wa Mlimba wote kwa tiketi ya Chadema na wenzao 37 wamerejeshwa rumande kufuatia hakimu wa kesi hiyo,  Ivan Msack kuwa mgonjwa.
Mbunge wa Mlimba, Suzan Kiwanga

Wabunge hao na wenzao leo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ambapo mahakama ilitakiwa kutoa uamuzi wa dhamana lakini imeshindikana hadi Desemba 8, 2017.

Hakimu wa mahakama hiyo Erick Rwehumbiza amesema hakimu Ivan amepata maradhi ya ghafla na yupo katika matibabu.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Peter Kibatala umesema kuhahirishwa kwa kesi hiyo na kutotolewa dhamana kwa washtakiwa kunalenga kuchelewesha upatikanaji wa haki.

 Awali Kibatala alitaka keshi hiyo iamishwe kwa hakimi mwingine lakini hoja yake hiyo ilipingwa na hakimu Rwehumbiza.

Jana Kulitokea mvutano kati ya upande wa mashtaka na ule wa utetezi kuhusu hati ya kiapo ya kupinga dhamana iliyowasilishwa mahakamani hapo.

Kutokana na mvutano wa kisheria, hakimu Ivan Msack aliahirisha kesi hiyo hadi leo Jumatano Desemba 6,2017 ili kutoa fursa kwa pande zote mbili kujibu hoja kuhusu hati hiyo.

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka nane likiwamo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.

Washtakiwa wanatetewa na mawakili Peter Kibatala, Ignas Punge, Fredrick Kiwelo na Bartholomew Tarimo.
Upande wa mashtaka unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Frederick Sumaye walihudhuria mahakamani.



Wengine waliofika mahakamani ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na wa Viti Maalumu, Devota Minja.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search