Mtanzania afariki ndani ya ndege akiwa amebeba dawa za kulevya...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MTU mmoja anayedaiwa kuwa ni mtanzania amekutwa amefariki ndani ya ndege akiwa amebeba dawa za kulevya tumboni.

Kamishna wa kupambana na dawa za kulevya, Rogers William Sianga 

Umauti huo umemkuta  ndani ya  ndege ya shirika la  ndege la Ethiopia na kwamba alikuwa akielekea nchini China.

Kamishna wa kupambana na dawa za kulevya, Rogers William Sianga amethibitisha taarifa hizo na kwamba uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo.

"Ni kweli hata sisi tumepokea taarifa za kifo hicho cha Mtanzania ndani ya ndege ya Ethiopia. Tunaendelea na mchakato wa kiuchunguzi,’’ amesema Sianga

Imeelezwa hivi sasa kumekuwapo na ongezeko la watanzania wanaotumika kusafirisha dawa za kulevya kwenda nje ya Tanzania.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search