Meya Mwita huyo Marekani...soma habari kamili na matukio360..#share
Na Christina Mwagala
MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo ameondoka kuelekea Chicago nchini Marekani kuhudhuria mkutano wa mameya duniani utakaofanyika Desemba 4 hadi 7, 2017.
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita
Mkutano huo unatarajiwa kuhusisha mameya 182 kutoka sehemu mbalimbali Dunia pamoja na mambo mengine watajadili suala la utawala bora na utumishi wa viongozi kwa wananchi.
Pia wataangalia na kujadili changamoto za majiji makubwa hususani katika sekta ya afya, miundombinu, maji safi na salama, elimu na mabadiliko ya tabia nchi.
Desemba 5, mameya wote waliohudhuria mkutano huo kwa pamoja watashindanisha majiji yaliyofanya vizuri katika sekta ya miundombinu. Jiji la Dar es Salaam limeingia kwenye ushindani huo kupitia mradi wa mabasi yaendayo haraka.
Katika ushindani huo, Meya Mwita amesema ana amini jiji la Dar es Salaam litaibuka mshindi wa tuzo hiyo kwa kuwa mradi huo umekuwa ukifanya vizuri katika sekta ya usafirishaji na watanzania wajiandae kupokea tuzo hiyo.
Majiji mengine ambayo yanameingia kwenye ushindani huo ni mji wa Cape Town na Cairo . Meya huyo atarajea nchini Desemba 8, 2017.
MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo ameondoka kuelekea Chicago nchini Marekani kuhudhuria mkutano wa mameya duniani utakaofanyika Desemba 4 hadi 7, 2017.
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita
Mkutano huo unatarajiwa kuhusisha mameya 182 kutoka sehemu mbalimbali Dunia pamoja na mambo mengine watajadili suala la utawala bora na utumishi wa viongozi kwa wananchi.
Pia wataangalia na kujadili changamoto za majiji makubwa hususani katika sekta ya afya, miundombinu, maji safi na salama, elimu na mabadiliko ya tabia nchi.
Desemba 5, mameya wote waliohudhuria mkutano huo kwa pamoja watashindanisha majiji yaliyofanya vizuri katika sekta ya miundombinu. Jiji la Dar es Salaam limeingia kwenye ushindani huo kupitia mradi wa mabasi yaendayo haraka.
Katika ushindani huo, Meya Mwita amesema ana amini jiji la Dar es Salaam litaibuka mshindi wa tuzo hiyo kwa kuwa mradi huo umekuwa ukifanya vizuri katika sekta ya usafirishaji na watanzania wajiandae kupokea tuzo hiyo.
Majiji mengine ambayo yanameingia kwenye ushindani huo ni mji wa Cape Town na Cairo . Meya huyo atarajea nchini Desemba 8, 2017.
No comments:
Post a Comment