Mzee miaka 73 aeleza yanayomkuta baada ya kuachiwa huru ....soma habari kamili na matukio

Na Mwajuma Juma, Zanzibar
MZEE wa miaka 73 Issa Mwema Issa ambae alidaiwa kutorosha msichana wa miaka 12 na kuhukumiwa kifungo cha miaka nane na kuachiwa huru amesema kuwa amekuwa katika  wakati mgumu  kutokana na kukosa ushirikiano kwa jamii tangu atoke jela.

Mwema ambae alitumikia kifungo hicho kwa muda wa miezi mitatu na kuachiwa huru  na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Makungu ambae alidai kuwa ushahidi wa kesi hiyo ulikuwa ni wa kupangwa.

Mzee Issa Mwema

Alisema kuwa pamoja na kuwa yupo huru lakini hana faraja kutoka kwa wanajamii wa hapo ikiwemo pia kukimbiwa na aliekuwa mke wake wa ndoa  ambae alidai  talaka na kumuacha.

“Nashukuru nimetoka jela lakini sina maisha ya furaha kwa jamii kwani imenitenga na sina ushirikiano wowote, hili limeniathiri, pia nimekosa mke”, alisema.

Alisema kuwa kabla hajafikwa na mkasa huo alikuwa ni mtu mashuhuri katika kijiji hicho kwa kushirikishwa katika shughuli zote za kijamii ikiwemo kusalisha na kuosha maiti lakini kwa sasa hashirikishwi kwa lolote


Hata hivyo alisema kuwa baada ya kuona hivyo ameamuwa kupumzika na kuacha shughuli  hizo zifanywe na watu wengine.

“Nimeamua niachane nayo kwani nimekuwa nikijiuliza wakati mimi sipo shughuli hizo zilikuwa hazifanyiki”, alisema Mzee Issa.

Alisema kuwa kuachiwa kwake huru hakumainishi kwamba alikuwa na uhusiano na jaji huyo na wala hakumshirikisha mtu yoyote katika kesi yake hiyo.

Hata hivyo alisema kuwa baada ya kupata matatizo hayo sasa hivi amekuwa na  woga mkubwa hata kumsaidia mtoto ambae atakuwa na tatizo kwa kuhofia kuwa amemfanyia udhalilishaji wa kijinsia.

“Mie nasema kuwa kwa sheria za ubakaji zilivyo kwa sasa hata ukimuona mtoto analia pale utaogopa kumsaidia au kumuuliza kwa kuhofia kuambiwa umembaka," alisema.

Hata hivyo Mwema aliongeza kwa kusema “na haya tujiepushe nayo kuwapa pesawatoto  kwa sababu akienda kwao ulikuwa ukilia umefanya nini hata kapigwa na mtoto mwenziwe lakini akionekana na pesa umempa wewe utaambiwa umembaka”.

Kwa mujibu wa Jaji Mkuu ambae alifanya mapitio jalada la kesi hiya ambayo ilihukumiwa katika mahakama ya wilaya Makunduchi alisema kuwa aliigunduwa kuwa ushahidi ni wa kupangwa na hakimu ambae aliihukumu kesi hiyo alitoa hukumu kwa presha za wanaharakati.



@@@@@@@@@@@2
caption
Issa Mwema Issa mzee alidaiwa kutorosha na kuachiwa huru na jaji mkuu wa Zanzibar kwa madai ushahidi wa kesi yake ni wa kupangwa akizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini  kwake Makunduchi kuzungumzia hali halisi ya kuachiwa kwake huru pamoja na kadhiya anayoipata
kutoka kwa jamii.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search