Naibu waziri akemea vitendo vya ushoga shule za dini...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Alex Stephen
SERIKALI imesema shule za taasisi za dini zimepoteza mwelekeo kwa kuanza kuzalisha vijana wa vijiweni na baadhi kujiingiza katika vitendo vya ushoga.

Naibu katibu mkuu wizara ya elimu, Dk Ave Maria Semakaf

Kauli hiyo imetolewa  leo na naibu katibu mkuu wizara ya elimu, Dk Ave Maria Semakaf wakati akifungua mkutano wa umoja wa shule za seminali na binafsi uliofanyika mjini Dodoma.

Semakafu alikemea tabia ya ushoga kuwa imeanza kuota mizizi kwani vijana wengi wa mitaani wakiulizwa mambo ya ushoga walijifunzia wapi wanazitaja shule za dini.


"Haya siyo maadili mliyokuwa mkifundisha tangu awali, kafundishe maadili ya kidini kama mlivyokuwa awali, tunapata malalamiko mengi kutoka kwa wazazi na wanafunzi wanaosoma huko kuhusu tabia hizo chafu,"amesema Semakaf

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search