Mkurugenzi Nkasi asimamishwa kazi, atuhumiwa kuchota bilioni 7...soma habari kamili na matukio360..#share
Alex Stephen
WAZIRI wa nchi ofisi ya rais Tamisemi, Seleman Jafo
amemsimamisha kazi mkurugenzi wa wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, Julius Kawondo kwa tuhuma za
rushwa na matumizi mabaya yaliyoisababishia
serikali hasara ya bilioni 7
Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo
Leo mjini Dodoma Jafo amewaambia waandishi wa habari kuwa
Kawondo ameshindwa kusimamia kile alichopaswa kukifanya kwa wakati katika eneo
lake la utumishi.
"Natumia sheria ya serikali za mitaa sura ya 4
kifungu cha kwanza hadi tano pamoja na sura ya 287 ya sheria hiyo ambavyo
vinanipa mamlaka hayo," amesema Jafo
Amesema fedha hizo zilikuwa za mradi wa maji wa kijiji
cha Kamwanda ambako mkurugenzi alishirikiana na mmoja wa maofisa kutoka wizara
ya maji.
Hivyo amemuomba waziri wa maji na umwagiliaji, Isaak Kamwelwe
kumchunguza mmoja wa watumishi katika wizara yake ambaye alishirikiana na mkurugenzi
huyo kuhujumu mradi wa maji katika kijiji cha Kamwanda wilayani humo.
Katika mkutano wa nane wa bunge, mbunge wa Nkasi
Kaskazini Ali Keissy alilalamika bungeni akimtaka rais akamkabidhi watumishi
wake kwani ni wabadhirifu.
Keissy alisema miradi ya maji ndiyo inaonekana kuhujumiwa
zaidi ikiwemo kununua vitu bandia na kufanya udanganyifu kwenye manunuzi




No comments:
Post a Comment