'Nchi yangu kwanza' kuzinduliwa Desemba 8...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

KAMPENI ya kitaifa ya uzalendo na utaifa ‘Nchi Yangu Kwanza’ inatarajiwa kuzinduliwa kupitia ‘usiku wa kitendawili’ Desemba 8, 2017 mjini Dodoma.
Rais John Magufuli (kushoto) na Mrisho Mpoto (kulia)

Usiku wa Kitendawili ulianzishwa baada ya msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto kuachia wimbo ‘Kitendawili’ na baadaye kufikiria kuanzisha usiku wa wimbo huo na kuanzisha mjadala kuhusu uzalendo.

Akizungumza  na Waandishi wa habari Msanii  wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto kupitia Kikundi cha Sanaa cha Mpoto Theatre Gallery na wadau wa sanaa za Ubunifu ambao ndio waratibu usiku huo na Wizara ya Habari Sanaa utamaduni na Michezo, amesema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli.

“Usiku wa kitendawili utatumika kama jukwaa la kuwaleta pamoja watanzania pamoja na viongozi wao ili kukumbushana kuhusu wajibu na kujadili mustakabali wa Taifa. Kutakuwa na vivutio mbalimbali pamoja na wimbo maalumu kutoka kwa wasanii maalumu Mwaka Huu,” amesema Mpoto.

Amesema lengo la kampeni hiyo ni kurejesha hali ya Uzalendo na Utaifa katika kutatua changamoto zinazojitokeza nchini na itakuwa ikifanyika kila mwaka sambamba na maadhimisho ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julis Kambarage Nyerere.

Amebainisha kwamba mambo ambayo yatafanyiwa kazi katika kampeni ni kudhibiti na kukomesha mmomonyoko wa maadili kwa viongozi wa Umma, rushwa, ufisadi, ubadhilifu wa mali za Umma na kuongeza hari ya kufanya kazi na Uzalendo.


Amesema baada ya uzinduzi huo  mwishoni mwa wiki hii mjini Dodoma, itafanyika kwenye mikoa yote nchini na itasimamiwa na Kamati za Utamaduni chini ya wenyeviti wakuu wa mikoa na wilaya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search