Nicol waomba Takukuru kuchunguza hasara bilioni 9...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu
WANAHISA wa kampuni ya uwekezaji ya Nicol, wameazimia uongozi uliopita, ukiongozwa na Felix Mosha ulipe gharama za kesi 41 walizozifungua katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa kama ilivyoamuriwa na mahakama hizo ama mali zao zifilisiwe.



Pia wameiomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuingilia kati na kuchunguza hasara ya bilioni 9.4  iliyopatikana mwaka 2009.
Mwenyekiti wa kampuni ya Uwekezaji wa Taifa (NICOL)  Dk Gideon Kaunda kulia na kushoto ni Mtendaji Mkuu  Adam Wamunza.


Maazimio hayo yamefikiwa Desemba 2, 2017 katika mkutano mkuu wa tatu wa mwaka wa wanahisa wa Nicol , ulifanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.
‘’ Pia tunataka wahusika wote waliofungua kesi katika mahakama mbalimbali waondoe kesi hizo   ndani ya mwezi mmoja  na ikishindikana menejimenti ichukue hatua.’’

Mwenyekiti wa bodi ya Nicol, Dk Gideon Kaunda alieleza kuwa uongozi uliokuwa ukiongozwa na Mosha ulisababisha hasara kufikia mwaka 2009  ya Sh 9.4 bilioni.

A,esema  Mosha aliiruka bodi yake na kufanya alivyotaka, kuupuza maagizo na miongozo mbalimbali iliyotolewa na mamlaka za udhibiti  kwa kutumia vibaya nafasi yake kama Mwenyekiti wa Nicol ikiwa ni pamoja na utekelezaji mbaya wa taratibu za bodi.

Aliongeza kuwa mamlaka ya masoko na mitaji ilimsimamisha kazi Mosha na bodi aliyokuwa anaiongoza lakini ilipuuza amri ya kusimamishwa  na kwamba kutokana na ujeuri huo na kwa madhumuni ya kuinusuru  kampuni wanahisa  waliomba na kupata ruhusa  ya mahakama kuutwaa uongozi wa Nicol  kwa madhumuni ya kiunda upya kwa kumteua, Interim Maneja  na kumpa jukumu la kuitisha mkutano wa dharura wa wanahisa.

“Mkutano huo uliitishwa Aprili 14,2012 wanahisa waliivunja bodi iliyokuwa inaongozwa na Mosha na kuteua bodi nyingine ambayo ilipewa jukumu la kukagua uwekezaji uliokuwa umefanywa , kutathmini  ‘viability ya Nicol’ na kuitisha mkutano mkuu wa wanahisa,’’ amesema Dk Kaunda.

Aliongeza kuwa  Mosha aligoma kutambua na kukubali maamuzi yaliyofanywa na wanahisa na akafungua moja kwa moja au kupitia mawakala kesi zaidi ya 41 katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa, kesi zote zililenga kumrudisha madarakani na kwamba aweze kudhibiti akaunti za Benki za Nicol.

Hata hivyo amesema Mosha hakuwahi kupata ushindi katika kesi zote hizo na kwamba uwepo wa kesi hizo uliathiri  bodi mpya katika utekelezaji wa majukumu iliyopewa na wanahisa.

Ilibainishwa kuwa pamoja na vikwazo hivyo, bodi mpya ilifanikiwa kuweka kumbukumbu sawa za wakurugenzi wa Nicol katika rejesta ya makampuni Brela, ilifanikiwa kulipa madeni yalikuwa yamefichwa na Mosha  ikiwa ni kumlipa mwanahisa chini ya makubaliano yaliyofikiwa katika kesi ya madai  namba 24,2013 dola za Marekani 2 milioni, zikiwa ni albaki ya dola milioni sita alizoipatia Nicol kufanikisha ununuzi wa hisa za  National Microfinance Bank.

Kulipa Sh 402,234,678.79 ikiwa ni malimbikizo  ya kodi ya pango  ya ofisi zilizotumiwa na Nicol kwa miezi 37 pamoja na kulipa deni la kodi za serikali  la Sh 556,785,241 na michango ya wafanyakazi  kwa akiba za uzeeni yaliyofikia Sh 249,514,422.

Dk Kaunda,  hata hivyo naye aliunga mkono uongozi uliokuwa ukiongozwa na Mosha walipe gharama hizo za kesi ambazo mahakama iliamuru walipe ama Mali zao zifilisiwe.

Jaji Mark Boman naye alipendekeza walipe gharama zote za  kesi na iwapo itashindikana Mali zao zifilisiwe.

Mwanahisa, Emmanuel David kutoka Arusha yeye aliomba wafilisiwe na wafikishwe mahakamani.

Mwanahisa Halidi Ramadhani yeye aliomba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru)  iingilie kati kuchunguza suala la upangaji wa ofisi ya Nicol katika Jengo la Raha Tower kama fedha hizo ni kweli zilipelekwa kwa wahusika ama mifukoni.

David Robi mwanahisa kutoka Mwanza yeye aliomba Mali zao zitambuliwe kwa kuwa mtoto akililia wembe ni lazima umkate kwa nini tunawahurumia na kwamba fedha zinazoendelea kulipwa zisitishwe.

Ilidaiwa kuwa pamoja ya kuwa hakuwahi kupata ushindi kwenye kesi hizo , uwepo wa kesi hizo uliathili bodi mpya katika utekelezaji wa majukumu iliyopewa na wanahisa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search