Samia Suluhu: Ukimwi unawaathiri zaidi wasichana, awaonya 'mashugadadi'...soma habari kamili na matukio360..#share

Salha Mohamed

TAKWIMU zinaeleza kuwapo kwa ongezeko  la takribani watu 9000 walioambukizwa  virusi vya ukimwi nchini kutoka mwaka  2013 watu 72,000  hadi  81,000 mwaka 2017. Waathirika zaidi ni wasichana wenye umri kati ya miaka 15-24.

Kufuatia hali hiyo makamu wa rais Samia Suluhu  amewaonya wanaume 'mashugadadi' kuacha kujihusisha na vitendo vya ngono na wasichana wadogo na kwamba watulizane na wavumilie kuwa na wake zao.
  
Makamu wa rais Samia Suluhu akihutubia hii leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya kilele cha siku ya ukimwi Duniani 

Takwimu hizo ni kati ya watanzania milioni 1.4 wanaoishi na virusi vya ukimwi huku waathirika  zaidi wakiwa ni wasichana wenye umri kati ya miaka 15-24.

Makamu wa rais, Samia Suluhu Hassan ameyasema hayo leo  jijini Dar es Salaam alipokuwa akizindua takwimu mpya za viashiria na ushamiri wa ukimwi Tanzania kwa mwaka 2016/2017 ikiwa ni kilele cha maandhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani.

“Takwimu zinaonesha baadhi ya mikoa inamaambukizi zaidi ya kiwango cha taifa cha asilimia 5 ambapo Mkoa wa Njombe una asilimia 11.4, Iringa asilimia 11.3, Mbeya asilimia 9.3,Mwanza asilimia 7.2, Kagera asilimia 6.5, Shinyanga asilimia 5.9 na Katavi kwa asilimia 5.9,”amesema.

Ameongeza mikoa mingine ni Songwe kwa asilimia 5.9, Rukwa asilimia 6.2, Dar es Salaam kwa asilimia 6.9, Ruvuma asilimia 5.6 na Pwani kwa asilimia 5.5.

Amesema bado kuna changamoto ya ulevi wa kupindukia na watu kufanya ngono zembe, kuwa na wapenzi wengi hivyo jamii inapaswa kuacha tabia hizo kwani serikali haiwezi kuyaingilia ni masuala binafsi.

Amefafanua kuwa mila hatarishi zimekuwa zikichangia maambukizi ya virusi vya ukimwi kama ngono na ndoa za utotoni ,kurithi wajane  kuacha.

Samia amewataka viongozi wa dini kuwaasa wanaume na vijana hasa wakike kutojiingiza kwenye janga hilo.

“Wanaume wote wa Tanzania mmekuwa na tamaa, muwe na maadili mnahisi wazee wenzenu wamechuja mnaenda kwa watoto mjue kuwa hili ni taifa letu …huu ni uuaji waacheni watoto wa kike waendelee na maisha,”amesema.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search