Wapinzani Zimbabwe wamshutumu Mnangagwa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mashirika ya Kimataifa
UPINZANI nchini Zimbabwe umelaumu kitendo cha rais mpya wa nchi hiyo, Emmerson Mnangagwa kuteua maofisa wakuu wa jeshi kuwa mawaziri katika baraza jipya alilolitangaza.
Rais wa Zimbabwe,Emmerson Mnangagwa.
Umedai  mabadiliko hayo ni kama usaliti wa matumaini miongoni mwa raia kutokana na kwamba vikosi vya usalama vilikuwa na nguvu nyingi wakati wa utawala wa Mugabe ambavyo hadi sasa vinaendelea kuthibiti taifa hilo.
Kiongozi wa upinzani, Tendai Biti amesema fungate iliokuwa ikisherehekewa Zimbabwe imeisha kabla ya kuanza.
Katika baraza hilo Mnangagwa amemteua ofisa mkuu wa jeshi kuwa  n awadhifu mkuu katika serikali yake.
Waziri mpya wa fedha ni Sibusiso Moyo ambaye ndie jenerali aliyetangaza katika runinga ya taifa hilo  kuwa jeshi limechukua udhibiti  na kumzuia nyumbani aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mubage.
Mkuu wa jeshi la angani, Perence Shiri ataongoza wizara ya fedha na kilimo.
Imedaiwa kuwa umoja ulioonekana katika siku za karibuni huenda ukabadilishwa na makabiliano ya uongozi katika uchaguzi wa mwaka ujao.
Rais Mnangagwa aliapishwa wiki moja iliopita kufuatia kujiuzulu kwa Robert Mugabe ambaye alikuwa mamlakani kwa takriban miaka 39.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search