Serikali isimamie majukumu yake ipasavyo...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

TUME ya haki za binadamu na utawala bora (THBUB), imekemea vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa haki za binadamu vinavyoendelea nchini.
Mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na utawala bora (THBUB) Bahame Nyanduga

Pia imeishauri serikali kuhakikisha inasimamia majukumu yake ili kukomesha vitendo hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya haki za binadamu ambayo hufanyika kila Desemba 10 iliyoandaliwa na kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) mwenyekiti wa THBuB Bahame Nyanduga, ametaja vitendo hivyo kuwa ni uminywaji wa uhuru wa kujieleza, siasa, watu kupigwa na kuumizwa, utekwaji na kupotea.

“Kwakeli tume inekemea jambo hili na Tunaishauri serikali kama ilivyo wajibu wake kwamba isimamie majukumu yake kuhakikisha vitendo hivi vinakomeshwa ili Tanzania isifikie mahali ikaonekana kama ni nchi ambayo haiheshimu haki za binadamu,” amesema.

“Kwa sababu hadi sasa sifa hiyo bado tunayo lakini naona taratibu sifa hiyo inaanza kuporomkoa,” ameongeza.

Nyanduga amesema tume haifurahishwi na vitendo hivyo na kwamba wamekuwa wakipokea malalamiko na kuyafanyia uchunguzi dhidi ya matukio hayo na kuyatolea matamko pamoja na kuishauri serikali ili ichukue hatua.

“Chamsingi naweza kusema ni kwamba kazi kubwa ya tume ni kuhakisha ina simamia misingi mbalimbali ya haki za binadamu na utawala bora ili tujenge jamii ineyoheshza binadamu imu haki,” amesema.

Amevitaka vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi haraka dhidi ya vitendo hivyo ili kuhakikisha haki inatendeka kwa waathirika wa vitendo hivyo , lakini pia mahakama zifanye kazi yake kwa uadilifu.

Amesema kulinda na kuheshimu haki za binadamu ni wajibu wa kila mtu na kueleza kuwa  serikali inawajibu mkubwa zaidi wa kuzilinda kwani ni mwanachama wa mikataba mingi ya kimataifa ya kuhusiana na masuala ya haki za binadamu.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search