Serikali yapiga marufuku matumizi fedha za kigeni...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI imesema wakati inaandaa mchakato wa mabadiliko ya sheria ya matumizi ya fedha za kigeni nchini, imepiga marufuku ununuzi na uuzaji kwa kutumia fedha hizo kuanzia Januari mosi, 2018.

Waziri wa fedha na mipango Dk. Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti ya serikali kwa mwaka 2017/18.

“Suala la matumizi ya fedha za kigeni sambamba na shilingi ya Tanzania  nchini, linasimamiwa na (a) sheria ya usimamizi wa fedha za kigeni ya mwaka 1992 (Tha Foreign Exchange Act, 1992, (b) Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2016 na (c) Tamko la serikali la mwaka 2007 kuhusu matumizi ya fedha za kigeni kulipia bidhaa na huduma katika soko la ndani,”

“Matumizi haya wakati wa kufanya miamala mbalimbali yanaweza kuwa na athari kiuchumi ikiwa ni pamoja na kudhoofisha thamani ya shilingi na sheria iliyopo kwa sasa  inasisistiza kuwa sarafu ya Tanzania ndiyo fedha halali na mtu au taasisi yoyote itakayokataa kupokea malipo kwa shilingi ya Tanzania atachukuliwa hatua za kisheria,” amesema.

Kufuatia hatua hiyo Dk. Mpango ametoa maagizo matano yanayotakiwa kizingatiwa kuanzia Januari 1, 2017, maagizo hayo ni bei zote hapa nchini zitangazwe kwa shilingi ya Tanzania. Bei hizo zitajumuisha kodi ya nyumba za kuishi na maofisi, bei ya ardhi, gharama za elimu na afya, vyombo vya usafiri na vifaa vya kielekroniki.

Mengine ni bei ambazo walengwa wake wakuu ni watalii au wateja wasio wakazi  zinaweza kutangazwa kwa fedha za kigeni na malipo yake yanaweza kufanyika kwa fedha za kigeni.

Bei  hizo zitajumuisha gharama za  usafirishaji kwenda nchi za nje kupitia Tanzania, gharama za mizigo bandarini kwenda nchi za nje, gharama za viwanja vya ndege na visa kwa wageni, na gharama za hoteli kwa watalii  kutoka nje ya nchi.

Ameongeza kuwa ni viwango vya kubadilisha fedha vitakavyotumika katika kuweka hizo bei katika sarafu mbili viwekwe wazi na visizidi vile vya nje.

Mengine ni mkazi yeyote wa Tanzania asilazimishwe kulipia bidhaa au huduma yoyote hapa nchini kwa fedha za kigeni na vyombo vya dola viwachukulie hatua kisheria wale wote watakaobainika kukiuka maagizo hayo ya serikali.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search