Zitto Kabwe amvaa rais Magufuli...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
KIONGOZI mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amemuomba rais John Magufuli kuweka tangazo lake wazi kwa umma la rasilimali na madeni alilowasilisha jana.
Kauli ya Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini inafuatia jana rais Magufuli kuwasilisha fomu yake ya tamko kuhusu rasilimali na madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo mtaa wa Ohio, jijini Dar es Salaam.
Zitto Kabwe
Leo katika ukurasa wake wa Twitter, Zitto ameandika: "Mmemwomba Rais aweke hilo tangazo lake wazi? Nadhani vyombo vya Habari mwende zaidi ya kuripoti ( kwa miaka zaidi ya 20 amekuwa akijaza fomu kama Waziri na baadaye Rais na pia wenzake waliomtangulia ). Twende hatua ya mbele zaidi, Mali hizi ziwekwe wazi na umma uchambue."
KIONGOZI mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amemuomba rais John Magufuli kuweka tangazo lake wazi kwa umma la rasilimali na madeni alilowasilisha jana.
Kauli ya Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini inafuatia jana rais Magufuli kuwasilisha fomu yake ya tamko kuhusu rasilimali na madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo mtaa wa Ohio, jijini Dar es Salaam.
Leo katika ukurasa wake wa Twitter, Zitto ameandika: "Mmemwomba Rais aweke hilo tangazo lake wazi? Nadhani vyombo vya Habari mwende zaidi ya kuripoti ( kwa miaka zaidi ya 20 amekuwa akijaza fomu kama Waziri na baadaye Rais na pia wenzake waliomtangulia ). Twende hatua ya mbele zaidi, Mali hizi ziwekwe wazi na umma uchambue."
Jana baada ya kuwasilisha fomu hiyo rais Magufuli aliipongeza sekretarieti hiyo kwa kazi inazofanya na kumtaka Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Harold Nsekela kutopokea fomu ya kiongozi yeyote ambaye atakuwa hajawasilisha tamko lake ifikapo tarehe 31 Desemba, 2017.
“Mhe. Jaji Nsekela ikifika tarehe 31 Desemba, ambayo ni siku ya mwisho kwa Mujibu wa sheria, weka mstari na usipokee fomu zingine, halafu tuone sheria itafanyaje, nakutakia kazi njema,” alisisitiza rais Magufuli.
Kwa upande wake Nsekela alimshukuru na kumpongeza Rais Magufuli kwa kutekeleza matakwa ya kisheria yanayomlazimu kujaza fomu hizo na amesisitiza kuwa ujazaji wa fomu hizo kwa viongozi wa umma siyo ombi.




No comments:
Post a Comment