Serikali yazionya taasisi za kidini...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Dar es Salaam
WIZARA ya mambo ya ndani ya nchi kitengo cha ofisi ya msajili wa jumuia za kidini imezionya taasisi za dini kufuata katiba zao na kwamba kujihusisha na siasa ni kinyume cha sheria.
WIZARA ya mambo ya ndani ya nchi kitengo cha ofisi ya msajili wa jumuia za kidini imezionya taasisi za dini kufuata katiba zao na kwamba kujihusisha na siasa ni kinyume cha sheria.
Wizara ya mambo ya ndani ya nchi
Taarifa iliyotolewa leo na katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (Mstaafu) inasema: "Baadhi ya Jumuia zimekuwa zikifanya shughuli zao kinyume na malengo yaliyomo kwenye Katiba zao bila kuiarifu Ofisi ya Msajili.
"Mathalani hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi wa Jumuia kutumia mahubiri yao wakati wa ibada kuchambua masuala ya siasa kinyume na Katiba zao kwani hakuna Jumuiya yoyote iliyosajiliwa chini ya Sheria ya Jumuiya ili kufanya kazi za siasa.
"Mathalani hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi wa Jumuia kutumia mahubiri yao wakati wa ibada kuchambua masuala ya siasa kinyume na Katiba zao kwani hakuna Jumuiya yoyote iliyosajiliwa chini ya Sheria ya Jumuiya ili kufanya kazi za siasa.
"Tabia hii ni kwenda kinyume na malengo na ni ukiukaji Kanuni ya 7 ya Kanuni za Jumuiya zilizoundwa chini ya Sheria ya Jumuiya, inayotamka kwamba Jumuiya yoyote hairuhusiwi kufanya mabadiliko ya malengo yake bila ya kibali cha Msajili."
Hata hivyo, Ofisi ya Msajili inazikumbusha
Jumuiya zote zinazofanya kazi kinyume na malengo yaliyoainishwa katika Katiba
zao zilizosajiliwa kuacha kufanya hivyo mara moja.
Inaeleza Ofisi ya Msajili inazikumbusha Jumuia zote kwamba ukiukaji wowote wa Sheria ni kosa ambalo linaweza kupelekea Jumuiya husika kufutiwa usajili wake kama ilivyoelezwa kwenye kifungu cha 17 cha Sheria husika.
No comments:
Post a Comment