Taasisi ya JK yawafanyia operesheni ya moyo watu 16...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ikishirikiana na taasisi ya Open Heart International (OHI) ya nchini Australia wamefanya upasuaji  wa  kufungua kifua kwa wagonjwa  16 wenye matatizo ya Moyo, kati ya hao watoto ni tisa

Madaktari wakifanya upasuaji

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo na kitengo cha Uhusiano na Masoko JKCI, upasuaji huo umefanyika katika kambi maalum ya matibabu ya Moyo iliyoanza Novemba 25, 2017 na kumalizika leo Desemba  01, 2017.

Wagonjwa watu wazima wamewafanyia upasuaji  wa kupandikiza mishipa ya damu kwenye moyo (CABG Coronary Artery Bypass Grafting) na kubadilisha milango ya moyo miwili hadi mitatu iliyokuwa imeziba au haifungi vizuri.

Kwa upande wa watoto wamefanya upasuaji na vipimo kwa watoto ambao vyumba vyao vya moyo havijakamilika na hivyo damu kwenda kwa wingi kwenye mapafu. Kuwafanyia watoto vipimo tukiwa tumefungua vifua inasaidia kufahamu aina ya upasuaji  tunaotakiwa kuufanya.

Upasuaji uliowafanywa kwa watoto ni wa awali  ili kuutayarisha moyo kwa ajili ya upasuaji mwingine ujao.

Watoto waliofanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ni wenye uzito wa kuanzia kilo nne hadi 12 ambao  umri wao ni miezi minne hadi miaka minne.

Kwa mara ya kwanza wameweza kufanya upasuaji kwa mtoto ambaye moyo wake ulikuwa upande wa kulia  na vyumba vyote vya moyo vinafanana wakati vinatakiwa kuwa tofauti .

Katika upasuaji huo wameweza kulinda mapafu yalikuwa yanapokea  damu kwa wingi kutoka kwenye mishipa ya moyo. Mtoto huyu pia tumeweza kumuwekea kifaa ambacho kitamsaidia moyo wake kufanya kazi vizuri (Pace Maker).

JKci imewashukuru  OHI kwa kuona umuhimu wa kushirikiana nao kutoa matibabu  kwa wagonjwa wenye matatizo ya moyo  paoja na kuwapatia mafunzo ambayo yamewasaidia  kuongeza ufanisi wa kazi.

Kabla ya kuanza kambi hiyo kulikuwa na mafunzo kwa wauguzi wa JKCI ambao walifundishwa jinsi ya kuwahudumia wagonjwa waliopo katika chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Wananchi wameombwa kuendela kuchangia damu kwani wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo wanahitaji kuongezewa damu  wakati wanapatiwa  matibabu.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search