TTCF: Sheria kudhibiti tumbaku itungwe....soma habari kamili na matukio360..#share

 Na Salha Mohamed, Dar es salaam
TANZANIA ndio nchi pekee Afrika Mashariki ambayo haina sheria ya kudhibiti matumizi ya tumbaku.

Pia kila mwaka takribani watu milioni 7 Duniani hufariki kutokana na matunizi ya tumbaku na  watu 700,000 wakivutishwa moshi wa tumbaku.


Mkurugenzi mtendaji wa chama cha kudhibiti Tumbaku Tanzania(TTCF) lutgard Kagaruki (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  kushoto ni mwandishi wa habari za uchunguzi, David Rwenyagira na Mwansheria wa kituo cha Sheria na haki za binadamu(LHRC), Tito Magoti.

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Kudhibiti Tumbaku Tanzania(TTCF)), Lutgard Kagaruki ameyasema hayo jijini Dar es Salaam

 “Tumeshtushwa na tamko la Waziri wa Kilimo, Charles Tizeba kuhusu mkataba wa kimataifa wa kudhibiti tumbaku wa shirika  la afya Duniani na ameubeza akidai unazuia kilimo cha tumbaku.’’ amesema Kagaruki na kuongeza “Nchi ilisaini mkataba huu mwaka 2007  ni wajibu kuutekeleza.”



Amesema utafiti unaonesha mwaka 2013 asilimia 14 ya watanzania ni wavutaji huku wanaume wakiwa na asilimia 2.9

 Amesema asilimia 17.5 ya wasiovuta sigara huvutishwa moshi wa tumbaku majumbani na asilimia 24.9 huvutishwa moshi huo  mahala pa kazi huku matokeo ya Global youth tobacco survey (2008) yakionesha asilimia 9.7 vijana ni wavutaji.

Amesema utafiti wa awali (2009) wa taasisi ya saratani ya ocean road unaonesha asilimia 32 ya saratani katika taasisi hiyo zilihusishwa na matumizi ya tumbaku zikiligharimu taifa dola za marekani milioni 40 kwa matibabu. 

"Pale Hospitali ya taifa Muhimbili,  utafiti ulibaini serikali ilikuwa inatumia dola za kimarekani milioni 186 kutibu magonjwa ya moyo yaliyohusishwa natumizi ya tumbaku, "amesema.

Amesema kilimo cha tumbaku  kinawaumiza wakulima kutokana na kemikali ya nikotini ambayo hupenya kwenye ngozi na hewa wanayovuta.



Amesema kilimo cha tumbaku bado kinaendelea kuongezeka kwa kasi na kwamba  kinanufaisha kampuni za tumbaku na si wakulima.


 Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Tito Magoti amesema mkataba huo haujalenga kuzuia, umelenga matumizi sahihi ya tumbaku. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search