Mohamed Salah mshindi tuzo ya BBC 2017...soma habari kamili na matukio360..#share

Na masharika ya kimataifa
MOHAMED Salah wa Misri amechaguliwa kuwa mshindi wa tuzo ya BBC kwa Mwanasoka bora wa Afrika Mwaka 2017.
Mohamed Salah

Nyota huyu wa Liverpool alipata kura nyingi zaidi ya Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon, Naby Keïta wa Guinea, Sadio Mané wa Senegal na mchezaji wa Nigeria Victor Moses.

"Nimefurahi sana kupata tuzo hii," mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliiambia BBC Sport.

"Huwa ni hisia ya kipekee unaposhinda kitu. Unahisi ulikuwa na mwaka mzuri sana. Kwa hivyo nina furaha sana. Ningependa kushinda tena mwaka ujao!"
Salah, aliyefunga mabao mengi zaidi ligi kuu England, akiwa na mabao 13, amekuwa na mwaka wenye mafanikio.


Mapema 2017 alikuwa nyota wa Misri walipochukua nafasi ya pili katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Baadaye mwakani, mshambuliaji huyu aliye na kasi alichangia katika magoli yote yaliyowasaidia Mafarao kufuzu kushiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1990 - aliwasaidia wenzake kufunga mabao mawili, naye akafunga mabao matano, moja ikiwa penalti kati yao na Congo iliyowawezesha kufuzu kwa fainali hizo za Urusi.

"Ninataka kuwa mwanakandanda bora zaidi wa Misri kwa hivyo mimi hutia bidii," anasema kijana huyu ambaye amekuwa raia wa tatu wa Misri kupata tuzo hii tangu 2008.


"Mimi hufuata njia yangu na ninataka watu wote Misri kufuata njia yangu"

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search