Tundu Lissu: Nilipoteza fahamu wiki mbili...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Nairobi
MWANASHERIA mkuu wa Chadema,
Tundu Lissu ambaye amekuwa akipokea matibabu Nairobi tangu alipopigwa risasi na
watu wasiojulikana mkoani Dodoma mwezi Septemba, amesema alipoteza fahamu wiki mbili.
Tundu Lissu akiwa hospitalini mjini Nairobi, Kenya akipatiwa matibabu
Akizungumza katika mahojiano
maalum na matukio360, mbunge huyo wa Singida Mashariki pia amesema anaamini kushambuliwa kwake kulihusiana
na siasa.
Akisimulia jinsi tukio la kupigwa
kwake risasi lilivyokuwa Tundu Lissu amesema ; ‘’Tulipofika karibu na nyumbani mara niliona gari aina ya Land
Cruiser Prado lenye rangi nyeupe likisimama pembeni yetu kuelekea mahala tulipotokea,
akashuka mtu mmoja, akaenda kuzungumza mlango wa mbele mara wakashuka watu wawili
wembamba wakiwa wamevalia kofia za kufunika sura zao wameshika ‘Shot Gun’.
‘’Mara nikasikia mlipuko puu,
baada ya hapo nikashtukia nipo Hospitalini Nairobi yaani nilipoteza fahamu kwa
wiki mbili.’’
Kuhusu mwenendo wa afya yake
amesema anaendelea kupata nafuu na muda
si mrefu hali yake itatengemaa na kuwa imara.
Pamoja na mambo mengine amelilaumu
Bunge la Tanzania akisema halijachukua hatua zozote kumsaidia tangu kulazwa
kwake hospitalini.
Hata hivyo amemshukuru makamu
wa rais Samia Suluhu na rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi kwa kumtembelea
hospitalini hivi karibuni.
Bunge la Tanzania limeshatoa ufafanuzi kuhusu suala hilo na
kwamba linafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.
Lissu ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani
alipigwa risasi zaidi ya thelathini na watu ambao mpaka sasa hawafahamiki pindi
alipokuwa mjini Dodoma akihudhuria vikao vya bunge.
Jeshi la polisi nchini lilisema upelelezi wa tukio
hilo unasuasua kutokana na dereva wa Mbunge huyo kutofika polisi kutoa
ushahidi.
Hata hivyo, taarifa kutoka Chadema zilisema dereva wa mbunge huyo yuko nchini Kenya kwa
ajili ya kupata matibabu ya kisaikolojia kutokana msongo wa mawazo alioupata
baada ya kisa hicho.
Lissu yuko nchini Kenya kwa takribani miezi mitatu
sasa ambako anapatiwa matibabu kutokana na majeraha ya risasi aliyoyapata
kutokana na shambulio hilo.
No comments:
Post a Comment