Kufungwa Man U Mourinho arushiwa vinywaji, alalamika...soma habari kamili na matukio360..#share

 Na mashirika ya kimataifa
MKUFUNZI wa Manchester United Jose Mourinho amerushiwa maji na maziwa kufuatia kushindwa na Manchester City huko Old Trafford jana.
Kocha Man U, Jose Mourihno

Hata hivyo Mourihno amelalamika timu yake kunyimwa penati kipindi cha pili kunako dakika ya 20 kabla ya mechi kumalizika na kwamba  Man u walistahili kupata penati na si kwa mchezaji wake  Ander Herrera kupewa kadi kwa kujiangusha kutokana na kuchezewa rafu na mchezaji wa Man City, Otamendi

“Ilikuwa ni penati ya wazi naamini tungetoka suruhu ya kufungana goli 2-2,’’ amesema Mourihno

Mashabiki Man  United walikasirika kutokana na kile walichokiona kuwa kusherehekea kupindukia kwa City kufuati ushindi wa Jumapili wa bao 2-1 ambalo lilifungua mwaka wa pointi 11 kileleni.

Wachezaji wa City walisherehekea na mashabiki wao baada ya kipenga cha mwisho na maafisa wengine wakajaribu kumshawishi meneja Pep Guardiola kujiunga nao lakini akakataa.

Baada ya wachezaji kuondoka uwanjani inaeleweka kuwa Mourinho alilalamika akiwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo kabla ya kurudi kwa mahojiano.

Upande wa City ulijibu huku kipa wa Brazil Ederson akijibizana na Mourinho kwa lugha ya kireno.


Goli la David Silva na Nicolas Otamendi jana yalizidi kuipa uongozi wa ligi Man City na kufikisha idadi ya mechi 40 bila kufungwa

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search