Ushahidi kesi ya Wema Sepetu kuanza kutolewa...soma habari kamili na matukio360..#share

Abdulrahim Sadiki,Dar es Salaam.

USHAHIDI  wa mashahidi wa upande wa mashtaka katika kesi inayomkabili msanii wa filamu, Wema Sepetu utaanza kusikilizwa Januari 10,2018 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.


Wema Sepetu

Leo kesi hiyo ilipaswa kuendelea kusikilizwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, Wakili wa Serikali, Costantine Kakula ameeleza  wapo tayari kwa ajili ya kuendelea na ushahidi na wana mashahidi wawili.

Kutokana na maelezo hayo, Wakili wa utetezi, Devotha Kianga kwa niaba ya Wakili Peter Kibatala ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.

Kwa kuwa wakili Kibatala  ambaye anawatetea,Wema na wenzake wawili, hakuwapo katika Mahakama ya Kisutu alikuwapo Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kwenye kesi namba 85 ya mwaka 2016.

Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Simba ameiahirisha kesi hiyo hadi Januari 10,2018.

Wengine wanaokabiliwa katika  kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Inadaiwa  kuwa  Februari 4,2017 katika Makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio  washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

 Kwa upande wa Wema yeye anadaiwa kuwa Februani Mosi, 2017 katika  eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam,  alitumia dawa za kulevya  aina ya Bangi.

Wema ni miongoni mwa watu waliotajwa na Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda wakituhumiwa kujihusisha na dawa za kulevya.

Inadaiwa kuwa Februari 3, 2017, Wema alijipeleka mwenyewe katika Kituo cha Polisi Kati ambapo alikamatwa.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search