Magufuli apiga marufuku kucheza ukiwa mtupu...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Dodoma
MWENYEKITI wa taifa wa CCM,
Dk John Magufuli amekemea vikali watu wanaocheza muziki wakiwa watupu ili kulinda maadili ya taifa.
Pia amewataka wadau wote
kulinda maadili ya watanzania na kwamba uchezaji muziki ukiwa mtupu ni kinyume
na maadili ya watanzania.
Mwenyekiti wa CCM taifa, John Magufuli
Ametoa agizo hilo leo mjini Dodoma
alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa jumuiya ya wazazi wa CCM. Katika mkutano
huo watachaguliwa viongozi wapya wa jumuiya hiyo
‘’Kila kitu kinamahala pake
hivyo haiwezekani watu wacheze wakiwa uchi katika muziki. Hili likemewe na
halipaswi kuchekelewa,’’ amesema Magufuli
Pia ameitaka jumuiya hiyo kuikemea
serikali kama itakwenda kinyume na
maadili.
‘’Pia wajibu wenu ni
kuikemea Serikali ikienda kinyume na maadili na pia mdhibiti na mkishindwa basi
mkemee uvunjifu wa maadili,’’ amesema.
Pamoja na mambo mengine
ameitaka jumuiya hiyo kuipa serikali shule inazozimiliki ili iziendeleze kwa
maslahi ya umma.
Amesema serikali ipo tayari
kuchukua angalau shule kumi kati ya 54 zinazomilikiwa na jumuiya hiyo na kwamba
serikali itawalipa fedha za ununuzi wa shule hiyo.
No comments:
Post a Comment