UTAFITI : Watu 9 uambukizwa virusi vya ukimwi kwa siku...soma habari kamili na matukio360..#share
Na Salha Mohamed
MATOKEO ya utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi (THIS) yameonesha watu
200 huambukizwa virusi vya ukimwi kwa siku nchini.
Waziri wa Afya,Jinsia na Maendeleo ya Jamii, Ummy Mwalimu
Utafiti huo ni kwa kipindi
cha mwaka 2016/2017. umefafanua kuwa watu 9
wanaambukizwa virusi vya ukimwi kwa saa.
Taarifa hiyo inasema
maambukizi mapya yapo zaidi kwa wanawake wenye umri kati ya miaka 25-34 kwa
asilimia 0.7.
Mbali na utafiti huo
kuonesha Tanzania imepiga hatua katika kupambana na ukimwi lakini bado kuna
changamoto katika kupambana na kumkinga mtoto asipate maambukizi kutoka kwa
mama yake katika kundi la wanawake walio katika umri wa kuzaa.
Tafiti hiyo inaonesha
kiwango cha maambukizi kwa watu wenye umri wa miaka 20 hadi 24 kuwa ni makubwa
kwa kundi la vijana hasa wasichana kuwa
na maambukizi mara mbili ya maabukizi ya wanaume.
Kutokana na hali hiyo,
utafiti huo umebainisha kuwa maambukizi hayo ni hatarishi hivyo kuhitaji
ubunifu katika kukabiliana na maambukizi mapya kwa vijana wenye umri kuanzia
miaka 20.
Matokeo hayo pia yameonesha
ukubwa wa maambukizi ya kaswende na homa ya ini aina ya B, kwa watu wenye umri
wa miaka 15 na zaidi.
Asilimia 5.6 ya watanzania
ya watu wenye umri wa miaka 15 na zaidi wamewahi kuugua kaswende.
No comments:
Post a Comment