Wakamatwa wakiwa na sare za JWTZ...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia Lainon Fratenus Lwegasira (20) mkazi wa Mahenge mkoani Morogoro na Noel Cleophace Wagesa (30) mkazi wa kigogo jijini Dar es Salaam kwa kosa la kukutwa wakiwa wamevaa sare za jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Katikati ni Lainon Fratenus Lwegasira (20), mmoja kati ya wawili waliokuwa na sare za JWTZ, akihojiwa na SACP Lazaro Mambosasa mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa Polisi Kanda hiyo SACP Lazaro Mambosasa, amesema watuhumiwa waliwakamata Desemba 15, 2017 majira ya saa 6:00 usiku eneo la Lugalo Kawe.

“Polisi wakiwa katika doria walifanikiwa kuwakamata vijana hao wakiwa wamevaa sare za JWTZ na kisu kimoja huku wakitumia gari no. T 306 CRU Toyota Carina rangi ya fedha,” amesema SACP Mambosasa.

Amesema kuwa watuhumiwa hao wanasadikiwa kujihusisha na matukio mbalimbali ya uporaji jijini humo, kabla ya ukamatwa kwao kulipatikana taarifa kuwa kuna watu wanne kati yao mmoja amevaa sare za jeshi na wanafanya uporaji ndipo askari walipofuatilia na kuwakamata.

Amesema watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa ili kubaini mtandao mzima na matukio yote waliyowahi kuyafanya. Na baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa watapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi nyingine za kisheria.

Mmoja wa watuhumiwa Lwegasira akihojiwa na kamanda Mambosasa alipozipata sare hizo, na alikuwa akizitumiaje, amedai kuwa alipewa na rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Frank.

Amesema alikuwa akizitumia katika kusafirishia mizigo hususani televisheni kutoka Zanzibar na kuzipeleka Tabata na amefafanua kwamba alikuwa akizivaa pindi wanaposafirisha mzigo kwenye gari ili wasikamatwe.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search